Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Makala & Uchambuzi Wadau wasisitiza kutunza amani Kenya
Makala & Uchambuzi

Wadau wasisitiza kutunza amani Kenya

Vurugu za mauaji ya Kenya yaliyowahi kutoka mwaka 2007
Spread the love

WITO wa amani umeendelea kutolewa kwa wananchi nchini Kenya kuelekea uchaguzi mkuu, ili kuepusha machafuko yaliyozuka katika uchaguzi wa mwaka 2007, anaandika Catherine Kayombo.

Miongoni mwa waliotoa wito huo ni Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi na Mipaka nchini Kenya, Wafula Chebukati kufuatia kifo cha aliyekuwa kaimu mkurugenzi wa masuala ya teknolijia katika tume hiyo, Christopher Musando.

Wafula amewataka Wakenya kuwa wavumilivu na kulinda amani, na kutoruhusu hasira na chuki kuwatawala.

“Tusipo angalia, tutaiweka nchi yetu matatani. Kama tume, tunaahidi kusimamia uchaguzi, kuondoka kwa musando kumerudisha hatua tulizopiga lakini haimaanishi hatutofanya kazi yetu”, aliwaambia wanahabari.

Wakati huo huo, muungano wa upinzani nchini Kenya, NASA umeitaka tume ya uchaguzi kumuajiri mtaalamu mpya wa kimataifa kutoka nje nchi ili kushughulikia idara ya teknolojia.

Haya yanajiri wakati mamia ya wanaharakati wa kutetea haki za binadamu waliandamana jana, Agosti mosi jijini Nairobi kulaani mauaji ya meneja huyo wa teknolojia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaMakala & Uchambuzi

Kanda ya Ziwa yaonyesha NMB inavyosaidia afya ya mama na mtoto

Spread the loveMafanikio inayozidi kupata Tanzania katika kupunguza vifo vya mama na...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

‘Mwanapekee’ wa Rais Samia: Atabadili nini Arusha?

Spread the loveMAPEMA wiki hii, baadhi ya viongozi walioapishwa na Rais Samia...

Habari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kipunguni waihoji serikali, ziko wapi fedha za fidia?

Spread the loveWATU wanaodai kwamba serikali ya Chama Cha Mapinduzi ni sikivu,...

Habari za SiasaMakala & UchambuziTangulizi

Askofu Bagonza: Tusichonganishwe; tusichokozane na tusikufuru

Spread the loveJOTO la chaguzi linapanda kila siku hapa nchini. Upo umuhimu...

error: Content is protected !!