Wednesday , 17 April 2024
Home Gazeti Makala & Uchambuzi Marekani, Uingereza kuchunguza kifo cha Musando wa Kenya
Makala & Uchambuzi

Marekani, Uingereza kuchunguza kifo cha Musando wa Kenya

Chris Musando, aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa Masuala Teknolojia wa Tume ya Uchaguzi na Mipaka Nchini Kenya (IEBC)
Spread the love

MAUAJI ya Kaimu Mkurugenzi wa Masuala Teknolojia wa Tume ya Uchaguzi na Mipaka Nchini Kenya (IEBC), yameziibua nchi za Marekani na Uingereza na kuamua kuungana na nchi hiyo kufanya uchunguzi wa kifo cha mtalaam huyo, anaandika Victoria Chance.

Chris Musando ambaye alikuwa msimamizi wa mifumo ya kompyuta ambayo ingesaidia kuzuia wizi wa kura wakati wa uchaguzi  mkuu unaotarajia kufanyika mwezi huu, aliuawa jumamosi iliyopita nchini humo.

Polisi wameeleza kuwa mwili wa Musando pamoja na mwanamke ambaye hakutambulika ulipatikana jijini  Nairobi, eneo la Kikuyu.

Gazeti la Daily Nation limeripoti kuwa Mabalozi wa Marekani nchini  Kenya, Robert Godec na Nic Hailey, wa Uingereza wamelaani mauaji hayo na kuongeza kuwa watashiriki katika uchunguzi huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

‘Mwanapekee’ wa Rais Samia: Atabadili nini Arusha?

Spread the loveMAPEMA wiki hii, baadhi ya viongozi walioapishwa na Rais Samia...

Habari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kipunguni waihoji serikali, ziko wapi fedha za fidia?

Spread the loveWATU wanaodai kwamba serikali ya Chama Cha Mapinduzi ni sikivu,...

Habari za SiasaMakala & UchambuziTangulizi

Askofu Bagonza: Tusichonganishwe; tusichokozane na tusikufuru

Spread the loveJOTO la chaguzi linapanda kila siku hapa nchini. Upo umuhimu...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rai ya Majaliwa kwa Watanzania

Spread the loveTAREHE 2 Aprili 2024, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alizindua mbio...

error: Content is protected !!