WITO wa amani umeendelea kutolewa kwa wananchi nchini Kenya kuelekea uchaguzi mkuu, ili kuepusha machafuko yaliyozuka katika uchaguzi wa mwaka 2007, anaandika Catherine Kayombo.
Miongoni mwa waliotoa wito huo ni Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi na Mipaka nchini Kenya, Wafula Chebukati kufuatia kifo cha aliyekuwa kaimu mkurugenzi wa masuala ya teknolijia katika tume hiyo, Christopher Musando.
Wafula amewataka Wakenya kuwa wavumilivu na kulinda amani, na kutoruhusu hasira na chuki kuwatawala.
“Tusipo angalia, tutaiweka nchi yetu matatani. Kama tume, tunaahidi kusimamia uchaguzi, kuondoka kwa musando kumerudisha hatua tulizopiga lakini haimaanishi hatutofanya kazi yetu”, aliwaambia wanahabari.
Wakati huo huo, muungano wa upinzani nchini Kenya, NASA umeitaka tume ya uchaguzi kumuajiri mtaalamu mpya wa kimataifa kutoka nje nchi ili kushughulikia idara ya teknolojia.
Haya yanajiri wakati mamia ya wanaharakati wa kutetea haki za binadamu waliandamana jana, Agosti mosi jijini Nairobi kulaani mauaji ya meneja huyo wa teknolojia.
Leave a comment