Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Maporomoko yaua watu 1000 Sierra Leone
Kimataifa

Maporomoko yaua watu 1000 Sierra Leone

Spread the love

IDADI ya watu waliofariki dunia kutokana na maporomoko ya udongo yaliyoambata na mafuriko katika mji wa milimani wa Regent nje kidogo ya Freetown nchini Sierra Leone imezidi elfu moja mpaka sasa, anaandika Victoria Chance.

Maporomoko hayo yaliambatana na mvua kali na mafuriko yaliyotokea wiki mbili zilizopita nchini Sierra Leone

Maofisa wa serikali ya Sierra Leone wamesema kuwa, idadi ya watu waliofariki dunia kutokana na maafa hayo ni zaidi ya elfu moja mpaka sasa hususani kwa kutilia maanani mamia ya watu waliotoweka na hawajulikani waliko hadi hii leo.

Hadi sasa zaidi ya watu 1000 wamethibitika kuwa waliaga dunia kutokana na maporomoko ya udongo ya mji wa Regent. Waziri mkuu wa freetown alitoa takwimu izo

Awali shirika la Hilali Nyekundu la Sierra Leone limetangaza kuwa watu wasiopungua elfu tatu wamepoteza makazi yao kutokana na maafa hayo ya maporomoko ya udongo na mafuriko katika mji wa milimani wa Regent nje kidogo ya Freetown na kwamba watu wengine 500 hawajulikani waliko.

Jeshi la Sierra Leone na timu za uokoaji zinaendelea na kazi ya kutafuta wahanga wa maafa hayo makubwa.

Rais Ernest Bai Koroma wa Sierra Leone ameomba misaada ya kimataifa kwa ajili ya wahanga wa maafa ya hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!