Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Maporomoko yaua watu 1000 Sierra Leone
Kimataifa

Maporomoko yaua watu 1000 Sierra Leone

Spread the love

IDADI ya watu waliofariki dunia kutokana na maporomoko ya udongo yaliyoambata na mafuriko katika mji wa milimani wa Regent nje kidogo ya Freetown nchini Sierra Leone imezidi elfu moja mpaka sasa, anaandika Victoria Chance.

Maporomoko hayo yaliambatana na mvua kali na mafuriko yaliyotokea wiki mbili zilizopita nchini Sierra Leone

Maofisa wa serikali ya Sierra Leone wamesema kuwa, idadi ya watu waliofariki dunia kutokana na maafa hayo ni zaidi ya elfu moja mpaka sasa hususani kwa kutilia maanani mamia ya watu waliotoweka na hawajulikani waliko hadi hii leo.

Hadi sasa zaidi ya watu 1000 wamethibitika kuwa waliaga dunia kutokana na maporomoko ya udongo ya mji wa Regent. Waziri mkuu wa freetown alitoa takwimu izo

Awali shirika la Hilali Nyekundu la Sierra Leone limetangaza kuwa watu wasiopungua elfu tatu wamepoteza makazi yao kutokana na maafa hayo ya maporomoko ya udongo na mafuriko katika mji wa milimani wa Regent nje kidogo ya Freetown na kwamba watu wengine 500 hawajulikani waliko.

Jeshi la Sierra Leone na timu za uokoaji zinaendelea na kazi ya kutafuta wahanga wa maafa hayo makubwa.

Rais Ernest Bai Koroma wa Sierra Leone ameomba misaada ya kimataifa kwa ajili ya wahanga wa maafa ya hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

error: Content is protected !!