Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kim Jong-un aitambia Marekani
Kimataifa

Kim Jong-un aitambia Marekani

Kim Jong-un, Kiongozi wa Korea Kaskazini
Spread the love

Kim Jong-un, Kiongozi wa Korea Kaskazini  amesema kuwa, vitisho vya hivi karibuni vya Rais Donald Trump wa Marekani dhidi ya nchi yake, ni vya kijinga, anaandika Hellen Sisya.

Kiongozi huyo amesema kuwa, vitisho hivyo ni kichekesho na ameonya kwamba, hadi sasa Marekani haijafahamu uwezo na nguvu kubwa ya Korea Kaskazini.

Amesisitiza kuwa , Pyongyang haiogopi Washington na kwamba, hata Maneva ya kijeshi ya Marekani yaliyofanyika hivi karibuni katika eneo la Korea na yale yanayoendelea sasa huko Australia, ni kujaribu tu kuonyesha uwezo wake uliozoeleka.

Eneo la Peninsula ya Korea limekuwa katika hali tete kutokana na siasa za uhasama zinazotekelezwa na Washington kwa kushirikiana na washirika wake kuilenga Korea Kaskazini. Kwa mara kadhaa Pyongyang imekuwa ikisisitiza kuwa, itaendelea kujiimarisha kijeshi madamu Washington itaendeleza vitisho vyake vya kila uchao dhidi yake katika eneo hilo.

Weledi wa mambo wanaamini kuwa, hadi sasa Marekani imefeli kwa kiasi kikubwa katika siasa zake za kupenda kujitanua kuihusu serikali ya Pyongyang na badala yake imebakia ikitumia shinikizo na vitisho pekee dhidi ya nchi hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!