Thursday , 18 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mabadiliko katika sekta ya madini
Habari Mchanganyiko

Mabadiliko katika sekta ya madini

James mdoe, Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini
Spread the love

Wizara ya Nishati na Madini imefanya mabadiliko kufuatia kupitishwa kwa sheria mpya ‘the written laws (miscellaneous amendmend ) Act 2017  iliyofanyiwa marekebisho kadhaa katika sheria ya mwaka 2010, anaandika Victoria Chance.

Marekebisho hayo ni kuanzishwa kwa tume ya madini, kufutwa kwa wakala wa ukaguzi wa madini, kuongezeka kwa malipo ya mrabaha asilimia nne(4%) hadi asiliia sita(6%), kwa madini ya metali na kuongeza kwa  kwa malipo ya mrabaha kutoka asilimia tano(5%) hadi sita(6%) kwa almasi na vito.

Pia kupitia marekebisho ya sheria ya fedha  na kodi, kila kampuni au mtu atakayesafirisha madini nje atalipia  ada ya ukaguzi ambayo ni asilimia moja ya thamani ya madini yake na hata wachimbaji wadogo  watalipia asilimia tano (5%) ya thamani ya madini yake ikiwa kama  kodi ya zuio.

Aidha, katika suala la kufutwa kwa  TMAA na ofisi za madini za kanda  wizara imesema watumishi wataendele  kufanya kazi kwani hawana tuhuma zozote na katika kipindi ambapo tume ya madini haijaundwa  shughuli za tume  zitafanywa chini ya kamishna wa madini .

Hata hivyo, wizara imewasisitiza wananchi kuendelea kutoa ushirikiano hasa katika  kipindi hiki cha mpito wakati serikali imesimamisha utoaji wa leseni za utafutaji na uchimbaji wa madini hadi hapo tume ya madini itakapoundwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

Habari Mchanganyiko

Serikali yatoa ajira watumishi 46,000, yatangaza utaratibu mpya kuajiri

Spread the loveSERIKALI imetangaza nafasi za ajira za watumishi wa umma 46,000...

error: Content is protected !!