MUDA wa kubembelezwa kwa Yahya Jammeh Rais wa Gambia aliyegoma kuondoka Ikulu ya nchi hiyo baada ya kuangushwa na mpinzani wake Adama Barrow sasa umekwishwa rasmi na muda wowote ataondolewa kwa nguvu, anaandika Wolfram Mwalongo.
Jeshi la Jumuiya ya Afrika Magharibi (ECOWAS) lipo tayari kupambana na Rais Jammeh ambapo kwa muwamjibu wa shirika la habari la Aljazeera kiongozi huyo aliongezewa muda kutoka jana hadi leo mchana.
Tayari majeshi ya ECOWAS yametua kwenye ardhi ya Gambia na kinachosubiriwa ni amri ya kuanza kwa mapambano ya kumtoa Jammeh Ikulu. Tayari wasaidizi muhimu wa rais huyo wameshamkacha na kujiweka kando na mkakati wake wa kung’ang’ania madaraka.
Edward Anthony Mwanasheria aliyekubali kumsimamia kesi yake kwenye Mahakama Kuu ya nchi hiyo kupinga matokeo ya uchaguzi wa mwaka jana sasa yupo uhamishoni.
Anthony alimwandikia barua mteja wake (Rais Jammeh) na kumsihi akabidhi madaraka kwa amani kwa aliyekuwa mpinzani wake Adama Barrow aliyetangazwa kushinda uchaguzi huo.
Tayari Rais Barrow ameapishwa rasmi kuwa rais wa taifa hilo ingawa hafla ya kuapishwa kwake imefanyika nchini Senegal ndani ya ubalozi wa Gambia.
Aidha, Jeshi la Gambia limesema lipotayari kumuunga mkono Rais Adama Barrow ambaye aliapishwa jana nchini Senegal.
Hata hivyo (ECOWAS) imesema Rais Jammeh hatakiwi kuendelea kubaki kwenye ardhi ya Gmabia kutokana na kuhofia usalama wake.
Leave a comment