Sunday , 2 April 2023
Home Kitengo Michezo Yondani kuikosa Singida United
Michezo

Yondani kuikosa Singida United

Spread the love

BEKI wa Yanga, Kelvin Yondani ataukosa mchezo Ligi Kuu Bara dhidi ya Singida United unaotarajia kuchezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam baaada ya kuoneshwa kadi tatu za njano katika michezo mitatu iliyopita. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Nahodha huyo ambaye alioneshwa kadi mfululizo katika michezo dhidi ya Stand United, Coastal Union na Mtibwa Sugar hivyo kutokana na kanuni za ligi hiyo atakosa mchezo unaofuata.

Katika hatua nyingine uongozi wa klabu hiyo umetoa taarifa ya kuwasamehe wachezaji Haji Mwinyi, Pius Buswita, Said Makapu na Ramadhani Kabwili baada ya kuomba msamaha kwa uongozi pamoja na benchi la ufundi kutokana na makosa ya utovu wa nidhamu.

Sababu za kabwili kuondolewa kwenye kikosi ni baada ya kuchelewa wakati wa kula timu ilipokuwa kambini, huku kwa upande wa wengine watatu walitakiwa kuwapo uwanjani wakati timu hiyo ilipokuwa ikiminyana na Stand United licha ya kutokuwa sehemu ya kikosi katika mchezo huo lakini waliamua kukaidi na kuingia mitini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!