Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Waliofariki MV Nyerere wafika 94
Habari MchanganyikoTangulizi

Waliofariki MV Nyerere wafika 94

Spread the love

IDADI ya watu waliofariki dunia katika ajali ya kivuko cha MV. Nyerere katika Ziwa Victoria jana. Anaripoti Mwandishi Maalum … (endelea).

Mpaka kufika saa 4 leo asubuhi pekee wameopolewa maiti 50 ambapo jioni jumla ya maiti 44 waliopolewa.

Watu 40 wanaripotiwa kuokolewa wakiwa hai mpaka sasa na wanaendele na matibabu.

John Mongella, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza anasema, utafutaji wa miili mingine unaendelea.

Viongozi mbalimbali wapo eneo la tukio wakiendelea na harakati za uokoaji.

Miili ya maiti hao imehifadhiwa kwenye Kituo cha Afya cha Bwisya kwa mujibu wa Mongella.

Kivuko cha MV. Nyerere kilizama jana ziwani humo ikiwani kilomita 50 kabla ya kutia nanga kwenye Kisiwa cha Ukara ilipokuwa ikielekea.

Raila Odinga, Kiongozi wa upinzani wa muungano wa NASA nchini Kenya amemtumia salama za pole Rais wa Tanzania na Wananchi wote kutokana na ajali ya MV. nyerere.

“Naomboleza na raia wa Tanzania katika kipindi hiki kigumu. Mungu awape amani na utulivu…” ameandika Odinga katika ukurasa wake wa Facebook.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!