KLABU ya Yanga inatarajia kucheza na timu ya Aigle Noir kutoka Burundi katika kilele cha Tamasha la Siku ya Mwananchi, linalotarajiwa kufanyika Jumapili 30, Agosti kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).
Tamasha hilo ambalo linafanyika kwa mwaka wa pili, huku likiwa na lengo la kutambulisha wachezaji wapya pamoja na wazamani watakaotumika katika msimu mpya ujao wa mashindano.
Timu hiyo ambayo inatarajia kutua nchini hivi karibuni, imeshika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu nchini Burundi katika msimu wa Ligi uliomalizika ikiwa na pointi 48.
Mchezo huo ambao unaweza kutumika kama kipimo kwa Yanga katika maandalizi yake kuelekea msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara unaotarajia kuanza 6 Agosti ambapo Yanga itashuka dimbani dhidi ya Tanzania Prison kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Yanga mpaka sasa imesajili jumla ya wachezaji 10 kutoka ndani na nje ya nchi huku ikiwa imeacha wachezaji 14, ambao walitumikia klabu hiyo katika msimu wa Ligi uliomalizika.
Leave a comment