Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wizara ya maji yaingia mkataba na GF Trucks
Habari Mchanganyiko

Wizara ya maji yaingia mkataba na GF Trucks

Spread the love

 

WIZARA ya Maji nchini Tanzania, imeanza mikakati ya kihakikisha inamaliza tatizo la maji mijini na vijijini kwa kuingia mkataba wa kusambaza vifaa vya maji na Kampuni ya GF Trucks & Equipment’s Ltd. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Mkataba huo umesainiwa leo Jumatano, tarehe 9 Februari 2022, jijini Dodoma baina ya Katibu Mkuu wa wizara hiyo Mhandisi Anthon Sanga na mkurugenzi wa kampuni hiyo, Imran Karmali.

Mhandisi Sanga amewataka walioshinda zabunu hizo za kusambaza vifaa hivyo kuhakikisha wanakamilisha na kukabidhi kwa wakati na isizidi mwezi wa tano ili kuendana na kasi ya Rais Samia Suluhu Hassani ya kuhakikisha miradi inamalizika kwa wakati.

Naye Karmali amesema wao wamelipokea agizo hilo la kukamilisha na kukabidhi vifaa hivyo kwa wakati.

Aidha ameishukuru Serikali kwa kuaminiwa na kwamba wao kama Kampuni hawataingusha katika hilo na ikiwezekana kabla ya mwezi wa tano kila kitu kitakuwa tayari, Ikizingatiwa GF inayomiliki kiwanda cha kutengeneza Magari hapa hapa nchini Tanzani kilichopo Kibaha mkoani Pwani wamejipanga vizuri.

Amesema, kupitia miradi ya maji wao itakuwa kazi nyepesi kwao kwani kupata kwa zabuni hiyo kutaongeza tija katika kiwanda chao na kwa kuwa wana wataalamu wa Kitanzania itakuwa rahisi kukamilisha mahitaji kwa wakati.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!