Friday , 10 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Watoto 37 wafariki kwa kusombwa na maji, Polisi watoa onyo
Habari Mchanganyiko

Watoto 37 wafariki kwa kusombwa na maji, Polisi watoa onyo

Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, David Misime
Spread the love

 

JESHI la Jeshi la Polisi Tanzania limetanga kuwa watoto 37 wamepoteza maisha katika matukio ya kusombwa na maji katika maeneo mbalimbali nchini kati ya mwezi Januari hadi Aprili mwaka huu. Anaripoti Abel Paul wa Jeshi la Polisi, Dar es Salaam … (endelea).

Pia Jeshi hilo linapenda tahadhari kwa wananchi wanatumia vibaya mitaandao ya kijamii hasa kipindi hiki cha mvua zinazoendela kunyesha kutoa taarifa mbalimbali ambazo siyo rasmi.

Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, SACP David Misime amesema matukio ya vifo vya watoto hao ambavyo vimetokena na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha yametokea katika baadhi ya mikoa ya Arusha, Dar es Salaam, Katavi, Kilimanjaro, Kigoma, Morogoro, Mwanza, Pwani na Rukwa.

Misime amebainisha kuwa matukio hayo kuna baadhi ya wazazi wanashindwa kuwalinda watoto wao ambapo amesema Jeshi hilo litaendelea kuwachukulia hatua za kisheria wale wote watakaobainika kushindwa kutekeleza wajibu wa kisheria na kusababisha mtoto kupata madhara.

Sambamba na hilo amesema kuwa Jeshi la Polisi nchini lingependa kutoa tahadhari na onyo kwa wale wachache wanaoendelea kutumia vibaya mitandao ya kijamii na kusababisha hofu, taharuki kwa wananchi.

Pia amesema kuwa kuna taarifa imerushwa hivi majuzi ikionyesha gari aina ya Toyota Land Cruiser hardtop ikisombwa maji ambapo mhalifu aliyetengeneza uongo huo aliandika tukio hilo limetokea muda mfupi huko Arusha, ambapo usahihi tukio hilo lilitokea mwaka jana nchini Sudan Kusini.

Aidha Misime amesema jamii iendelee kuwakumbusha watumiaji vibaya wa mitandao ya kijamii kuwa baadhi ya binadamu wenzao wana magonjwa na wanapopata taarifa za kushtua kama hizo wanaweza kupata madhara makubwa zaidi hata kupoteza maisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC, Wizara ya Katiba wajadili uanzishaji haki binadamu katika biashara

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umefanya...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Sitta ang’ang’ana wanafunzi watibiwe bure, Serikali yagoma

Spread the loveMBUNGE wa Urambo, Margaret Sitta, ameishauri Serikali iweke utaratibu wanafunzi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Waitara ahoji bungeni mwarobaini mauaji katika mgodi Barick North Mara

Spread the loveMBUNGE wa Tarime Vijijini (CCM), Mwita Waitara, ameitaka Serikali kutafuta...

Habari MchanganyikoMichezo

Arafat atoka bima na kurejea kwenye benki

Spread the loveRais wa Zanzibar Hussein Mwinyi amemteua Arafat Ally Haji kuwa...

error: Content is protected !!