Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Watalaam ugonjwa wa Ini kujifua India
Afya

Watalaam ugonjwa wa Ini kujifua India

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma Muhimbili, Aminiel Aligaesha
Spread the love

HOSPITALI ya Taifa Muhimbili inatarajia kuwapeleka nchini India watalaam mbalimbali katika sekta ya afya kwa ajili ya mafunzo ya ugonjwa wa Ini, anaandika Angel Willium.

Watalaam hao ni pamoja na madakatari saba, wauguzi wawili pamoja na mhandishi wa vifaa tiba ambao watakaa huko kwa muda wa miezi mitatu.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma, Aminiel Aligaesha amesema, madakatari hao wanatarajia kuondoka Novemba 29, mwaka huu na watakaporudi wataongeza ufanisi katika kufanya uchunguzi na tiba ya ugonjwa wa Ini na kuondoa uvimbe mkubwa unaodhoofisha afya ya mgonjwa.

“Mafunzo hayo yatachukua miezi mitatu, na watarejea nchini wiki ya kwanza ya mwezi machi mwaka 2018, lengo ni kujenga uwezo wa ndani utakaowezesha upandikizaji wa Ini kwa mgonjwa”amesema Aligaesha.

Aidha, Aligaesha amesema upatikanaji wa huduma hizi hapa nchini, utasaidia kwa kiwango kikubwa kuokoa na kuboresha maisha ya mgonjwa.

Mmoja wa madaktari wanaotarajia kwenda kwenye mafunzo, John Rwegasha ambaye anatibu ugonjwa wa mfumo wa chakula na Ini amesema anashukuru uongozi wa hospitali kuchagua kitengo chao kwenda nchini India.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

Songwe katika mikakati ya elimu ya lishe kudhibiti udumavu

Spread the love  SERIKALI mkoani Songwe imejipanga kuendelea kutoa elimu ya lishe...

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

error: Content is protected !!