Tuesday , 30 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900
AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu
Spread the love

SERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya ngazi ya jamii, kwa kuanza kutoa mafunzo ya wahudumu wa afya ngazi ya jamii kwa watu takribani 8,900 kwenye mikoa 10. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, leo tarehe 8 Aprili 2024, kupitia ukurasa wake wa Twitter, amesema watakaohitimu mafunzo hayo wataajiriwa serikalini. Amesema watu wenye ujuzi wa afya hawatahusika katika mpango huo.

“Afya ya jamii, nyumba kwa nyumba, kitongoji kwa kitongoji, mtaa kwa mtaa, hatumuachi mtu nyuma. Fursa kwa wananchi wenye umri kuanzia miaka 18 hadi 55, watakaochaguliwa tutawapa mafunzo maalum ya miezi sita (miezi mitatu darasani, miezi mitatu mafunzo) na Serikali itadhamini mafunzo haya,” ameandika Ummy na kuongeza:

“Baada ya mafunzo tunatoa ajira kwao ili waweze kufanya kazi katika vitongoji vyao na mitaani kwao. Lengo kumfikia kila mtanzania alieko mjini au kijijini na huduma bora za afya.”

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Wizara ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI, mikoa 10 itakayonufaika katika awamu ya kwanza ya mpango huo ni Geita ambayo itapata wahudumu 920. Kagera (878), Kigoma (1,094), Lindi (1,724), Mbeya (836), Njombe (746), Pwani (480), Songwe (774), Tabora (966) na Tanga (482)

Taarifa ya TAMISEMI imebainisha kuwa, lengo la mpango huo ni kupata wahudumu wawili wa afya ngazi ya jamii, ambao ni mwanamke na mwanaume.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

7 wafa Ulanga, mbunge alia kutelekezwa na mawaziri, Tanroad

Spread the loveWatoto saba wamepoteza maisha na zaidi ya kaya 70 kukosa...

Habari za SiasaTangulizi

Wizara Katiba na Sheria yaliomba Bunge Sh. 441.2 bilioni

Spread the love  WIZARA ya Katiba na Sheria imeliomba Bunge liidhinishe bajeti...

error: Content is protected !!