Wednesday , 8 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Washukiwa 15 mauaji kanisani Sri Lanka wauawa
Kimataifa

Washukiwa 15 mauaji kanisani Sri Lanka wauawa

Spread the love

WATU 15 wanaoshukiwa kuhusika katika shambulio la kigaidi lililopoteza maisha ya watu 253 kwenye makanisa nchini Sri Lanka, wameuawa katika majibizano ya risasi. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Watu hao wanaodaiwa kuwa wanamgambo wa dola la Kiislamu (ISIS) wameuawa huku wengine wakitokomea kusikojulikana  baada ya jeshi la polisi jana kuvamia makazi yao.

Kwa mujibu wa mitandao ya kimataifa, Jeshi la Polisi lilipovamia makazi hayo yaliyoko mashariki mwa Sri Lanka mjini Sainthamaruthu, walikuta milipuko mitatu, sare na bendera za ISIS.

Aifsa wa Polisi Sri Lanka, Meja Jenerali, Aruna Jayasekera   amesema watu sita kati ya 15 waliouliwa ni washukiwa wa moja kwa moja wa tukio hilo lililotokea siku ya Pasaka tarehe 21 Aprili 2019, na wengine tisa ni raia wa kawaida wakiwemo watoto.

Meja huyo amesema, polisi wanaendelea na uchunguzi kuhusu madai ya raia kushirikiana na wanamgambo wa ISIS.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!