Tuesday , 30 May 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Washukiwa 15 mauaji kanisani Sri Lanka wauawa
Kimataifa

Washukiwa 15 mauaji kanisani Sri Lanka wauawa

Spread the love

WATU 15 wanaoshukiwa kuhusika katika shambulio la kigaidi lililopoteza maisha ya watu 253 kwenye makanisa nchini Sri Lanka, wameuawa katika majibizano ya risasi. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Watu hao wanaodaiwa kuwa wanamgambo wa dola la Kiislamu (ISIS) wameuawa huku wengine wakitokomea kusikojulikana  baada ya jeshi la polisi jana kuvamia makazi yao.

Kwa mujibu wa mitandao ya kimataifa, Jeshi la Polisi lilipovamia makazi hayo yaliyoko mashariki mwa Sri Lanka mjini Sainthamaruthu, walikuta milipuko mitatu, sare na bendera za ISIS.

Aifsa wa Polisi Sri Lanka, Meja Jenerali, Aruna Jayasekera   amesema watu sita kati ya 15 waliouliwa ni washukiwa wa moja kwa moja wa tukio hilo lililotokea siku ya Pasaka tarehe 21 Aprili 2019, na wengine tisa ni raia wa kawaida wakiwemo watoto.

Meja huyo amesema, polisi wanaendelea na uchunguzi kuhusu madai ya raia kushirikiana na wanamgambo wa ISIS.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Mkutano wa Quad Hiroshima waibuka na kutafuta amani na ustawi wa Indo-Pacific

Spread the love  JITIHADA za mazungumzo ya Pande Nne (Quad), hazikuthaminiwa na...

KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Spread the love  MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya...

Kimataifa

Kiwango cha ukosefu wa ajira nchini China chaongezeka

Spread the love  WAKATI kiwango cha ukosefu wa ajira kwa vijana nchini...

Kimataifa

Kampuni za kigeni zahofia kuendelea na biashara China

Spread the love OPERESHENI ya kiuchunguzi inayofanywa na Serikali ya China kwa...

error: Content is protected !!