Wednesday , 27 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Kimbunga cha Keneth: Mtwara, Lindi yapumua
Habari Mchanganyiko

Kimbunga cha Keneth: Mtwara, Lindi yapumua

Spread the love

MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imewataka wananchi wa mikoa ya Lindi na Mtwara kuendelea na shughuli zao, huku ikiwatahadharisha kufuatilia utabiri utakaotolewa kila mara kuhusu Kimbunga Kenneth. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kauli hiyo ya TMA imekuja baada ya Kimbunga Kenneth kilichotabiriwa kutokea katika mikoa hiyo Alhamisi ya terehe 25 Aprili 2019 na kuleta athari, kubadili mwelekeo wake na kwenda katika maeneo ya Kusini mwa Pwani ya nchi ya Msumbiji.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana tarehe 26 Aprili 2019, Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dk. Agnes Kijazi, amesema kimbunga Kenneth bado kipo katika ardhi ya Msumbiji na mwishoni mwa wiki kinatarajiwa kurudi baharini.

Dk. Kijazi amesema kimbunga hicho kitakaporejea baharini kinaweza leta athari katika mikoa hiyo kama ilivyotabiriwa awali na TMA. Hata hivyo, amesema mamlaka hiyo itaendelea kufuatilia kwa ukaribu kimbunga hicho na kutoa taarifa kwa umma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari Mchanganyiko

Wizara ya madini kurusha ndege ya utafiti wa madini Geita

Spread the loveKutokana na mchango wa wachimbaji wadogo wa madini kwenye pato...

Habari Mchanganyiko

Jafo aagiza kampuni za madini kuzingatia utunzaji mazingira, azitaka zijifunze kwa GGML

Spread the loveWAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia apewa tano ujenzi barabara Mtwara

Spread the loveWANANCHI wa Mkoa wa Mtwara, wameishukuru Serikali ya Rais Dk....

error: Content is protected !!