Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Kimbunga cha Keneth: Mtwara, Lindi yapumua
Habari Mchanganyiko

Kimbunga cha Keneth: Mtwara, Lindi yapumua

Spread the love

MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imewataka wananchi wa mikoa ya Lindi na Mtwara kuendelea na shughuli zao, huku ikiwatahadharisha kufuatilia utabiri utakaotolewa kila mara kuhusu Kimbunga Kenneth. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kauli hiyo ya TMA imekuja baada ya Kimbunga Kenneth kilichotabiriwa kutokea katika mikoa hiyo Alhamisi ya terehe 25 Aprili 2019 na kuleta athari, kubadili mwelekeo wake na kwenda katika maeneo ya Kusini mwa Pwani ya nchi ya Msumbiji.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana tarehe 26 Aprili 2019, Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dk. Agnes Kijazi, amesema kimbunga Kenneth bado kipo katika ardhi ya Msumbiji na mwishoni mwa wiki kinatarajiwa kurudi baharini.

Dk. Kijazi amesema kimbunga hicho kitakaporejea baharini kinaweza leta athari katika mikoa hiyo kama ilivyotabiriwa awali na TMA. Hata hivyo, amesema mamlaka hiyo itaendelea kufuatilia kwa ukaribu kimbunga hicho na kutoa taarifa kwa umma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!