Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Wapiga kura wampokea kishuja Odinga, wasukuma gari
Kimataifa

Wapiga kura wampokea kishuja Odinga, wasukuma gari

Spread the love

 

MGOMBEA urais wa muungano wa Azimio la Umoja, Raila Odinga mapema leo saa 4:00 asubuhi amewasili katika Shule ya msingi ya Old Kibra ambayo ndio kituo chake cha kupiga kura na kupokewa kishujaa na maelfu ya wapiga kura nchini Kenya. Anaripoti Mwandshi Wetu, Kenya … (endelea).

Raila ambaye ni mmoja kati ya wagombea wanne wa uchaguzi wa urais mwaka 2022, amekuwa wa mwisho kupiga kura yake baada ya awali wagombea wengine kama William Ruto wa UDA akiwa wa kwanza kupiga kura yake eneo la Sugoi.

David Mwaure wa Agano alipiga kura yake pia maeneo ya Upperhill Nairobi akifuatiwa na wakili msomi George Wajackoyah ambaye alifika maeneo ya Matungu dakika chache mbele ya Odinga.

Hata hivyo, Wajackoyah alishindwa kupiga kura kwa wakati baada ya mtambo wa KIEMS kushindwa kumtambua na kumfanya asubiri kwa muda zaidi ili kuona kama atapiga kura.

Raila aliwasili katika kituo hicho huku akilakiwa na mamia ya wafuasi wake waliomsubiri kwa mbwembwe kumkaribisha Old Kibra na baada ya kupiga kura walimsindikiza kwa kulisukuma gari lake hadi nje ya kituo hicho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!