WAPALESTINA waishio katika Ukanda wa Gaza, wameanza kukimbia makazi yao baada ya Israel kuwapa saa 24 wakitaka wahamie sehemu nyingine ili kupisha mashambulizi yake. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).
Mtandao wa BBC Swahili umeripoti kuwa, leo Ijumaa, wananchi wa Gaza wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 1,000,000, baadhi yao wameanza kupakia mizigo yao na kuhakama kueleka kusini walikoamriwa kwenda kupata hifadhi na Israel.
Israel ilitoa agizo hilo kwa raia wa Gaza kuyahama makazi yao, ikiwa ni muda mfupi tangu isitishe kupeleka huduma muhimu kwenye eneo hilo ikiwemo chakula, mafuta na umeme.
Pia, imeahidi kufanya mashambulizi mfululizo hadi pale kundi la wanamgambo la Hamas la Palestina, litakapowaacha watu zaidi ya 100 waliowaweka mateka.
Wakati hayo yanajiri, Umoja wa Mataifa (UN), umesema wananchi wa Gaza wanakabiliwa na hali ngumu ya kimaisha baada ya kukosa huduma muhimu, huku wajawazito 50,000 wakitajwa kuwa hatarini kufuatia mapigano yanayoendelea.
Tayari ofisi ya UN ya kuratibu masuala ya kibinadamu, imetoa wito kwa nchi wanachama kutoa msaada wa Dola za Marekani 294 milioni, kwa ajili ya kuwapa mahitaji ya dharura Wapalestina.
Mpaigano hayo yameibuka baada ya Hamas kufanya shambulio la kushtukiza upande wa Israel, liliopoteza maisha ya watu 900 waliokuwemo katika sherehe. Kufuatia shambulizi hilo, Israel imeendelea kufanya mashambulizi kulipa kisasi.
Leave a comment