Wednesday , 6 December 2023
Home Kitengo Maisha Afya Wananchi Ileje waiangukia serikali ukamilishaji wa zahanati
Afya

Wananchi Ileje waiangukia serikali ukamilishaji wa zahanati

Spread the love

Wananchi wa kijiji cha Mbembati kata ya Lubanda wilaya ya Ileje mkoani Songwe wamejenga zahanati ya Kijijini hapo kwa nguvu zao ili kupunguza adha ya kusafiri umbali wa kilomita nane kufuata huduma katika kituo cha afya Lubanda. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe…(endelea).

Wananchi hao walianza ujenzi wa zahanati hiyo mwaka 2014 kwa lengo la kuwapunguzia akina mama wajawazito ambao walikuwa wakijifungulia njiani na majumbani wakati wakifuata huduma ya uzazi kituo cha afya Lubanda ambapo awali ilikuwa zahanati.

Akisoma taarifa ya kijiji, Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Odeni Kandonga  amesema kati ya fedha hizo wananchi wamechangia milioni 15.6, fedha ya mfuko wa jimbo ni milioni nne, na michango ya wahisani ni Sh 800,000.

Akijibu ombi la wananchi wa kijiji hicho Mkuu wa Wilaya hiyo, Farida Mgomi amewapongeza wananchi kwa kutumia nguvu zao kushiriki ujenzi huo kwa kuchangia fedha na kuahidi kuwa zahanati hiyo itakuwa  ni mwarobaini wa kupata huduma za afya karibu pindi itakapoanza kutoa huduma

“Kutokana na mwitikio wenu Serikali itahakikisha inawaunga mkono kumalizia sehemu iliyobaki hivyo basi mhandisi wa ujenzi atakuja wiki ijayo kufanya tathmini ya eneo la zahanati ilipobaki ili jengo hilo liingizwe kwenye bajeti kwa ajili ya kutenga fedha za kukamilisha na huduma zianze kutolewa,” amesema Mgomi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

RAS Songwe: Tumepigwa… mkurugenzi nakupa siku 21

Spread the loveKATIBU tawala mkoani Songwe, Happines Seneda ametoa siku 21 kwa...

AfyaHabari Mchanganyiko

Majaliwa aipongeza GGML mapambano dhidi ya Ukimwi

Spread the loveWaziri Mkuu Kassim Majaliwa ameipongeza Kampuni ya Geita Gold Mining...

AfyaHabari Mchanganyiko

GGML waungana na Biteko kuanika mbinu za mapambano dhidi ya Ukimwi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

AfyaMichezo

GGML yatoa milioni 17 kung’arisha ATF Marathon

Spread the loveKATIKA kuendelea kuunga mkono jitihada za Serikali kukabiliana na maambukizi...

error: Content is protected !!