Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Biashara Wamachinga Kivule wamwangukia Rais Samia
Biashara

Wamachinga Kivule wamwangukia Rais Samia

Wamachinga
Spread the love

WAFANYABIASHARA ndogondogo (wamachinga), katika eneo la Kivule jijini Dar es Salaam, wamemuomba Rais Samia Suluhu Hassan, awasaidie ili wapate mali zao zinazodaiwa kuchukuliwa na baadhi ya mgambo waliovunja vibanda vyao usiku wa kuamkia jana Jumanne. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Ombi hilo limetolewa na wafanyabiashara waliokumbwa na kadhia hiyo wakati wakizungumza na waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam.

Wamedai kuwa, vibanda vyao vya biashara vimevunjwa kinyume cha sheria na baadhi ya viongozi wanaowalazimisha kwenda katika soko ambalo wanadai halina miundombinu mizuri ya wao kufanya biashara.

Mmoja kati ya wamachinga waliokumbwa na mkasa huo, Yusuph Mkuku, amesema “tunapenda kuiambia serikali kwamba kuna watu ambao wameanzisha soko lao kinyume cha sheria wametuma watu kuja kutuvunjia vibanda vyetu wakitulazimisha kwenda katika soko lao ambalo ili upate kizimba unatakiwa utoe Sh. 350,000 kwa mwezi.”

“Wanalitumia soko hilo kujinufaisha wenyewe lakini pia halina miundombinu mizuri ya kuvutia wateja kwanza ni chafu sana. Namuomba mama Samia atusaidie turudishiwe mali zetu mfano mimi nimeibiwa kuku 20 na waliochukua ni wale waliovunja vibanda,” amesema Mkuku.

Mwanaharakati huru, Bihimba Mpaya amewataka viongozi wa eneo hilo kutowasumbua wafanyabiashara ambao wamejitoa kwa ajili ya kutafuta ridhiki kihalali.

“Muda umefika sasa tunawataka walioiba mali zetu na tunawajua wako hapa KIvule, wazirudishe. Tunaita wezi kwa sababu hamuwezi kuvunja vibanda usiku bila sababu za msingi wakati vimejengwa katika maeneo sahihi,” amesema Bihimba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Biashara

Cheza sloti ya Zombie Apocalypse na ushinde kirahisi

Spread the love Wengi wetu hupenda filamu za Mazombie huwa zinatishakidogo lakini...

Biashara

Ushirikishwaji wa wafanyakazi ni muhimu katika utekelezaji wa sera za afya na usalama kazini

Spread the love  KILA ifikapo Aprili 28 ya kila mwaka, dunia huadhimisha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Biashara

Wazir Jr kinara wa ufungaji KMC FC ajiunga Meridianbet

Spread the love    MUITE Wazir Jr ‘The King of CCM Kirumba’,...

error: Content is protected !!