Monday , 11 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Bunge latakiwa kudhibiti unyanyasaji kwa wafugaji
Habari Mchanganyiko

Bunge latakiwa kudhibiti unyanyasaji kwa wafugaji

Mifugo
Spread the love

MASHIRIKA Yasiyo ya Kiserikali (NGO’S), 16 yakiongozwa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), wameliomba Bunge lichukue hatua ili kulinda haki za wafugaji waishio karibu na hifadhi za taifa, ambao wanadaiwa kufanyiwa vitendo vya ukatili ikiwemo kuporwa mifugo yao na baadhi ya maafisa uhifadhi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Wito huo umetolewa leo tarehe 8 Novemba 2023 na Mkuu wa Idara ya Utetezi kwa Watetezi wa Haki za Binadamu THRDC, Paul Kisabo, akisoma tamko la mashirika hayo, jijini Dar es Salaam.

“Ni wakati sasa Bunge letu lichukue hatua sababu wabunge wamekuwa wakilalamika bungeni lakini hakuna mafanikio hivyo Bunge lihakikishe linalinda maslahi ya wananchi ambao linawawakilisha,” amesema Kisabo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jukwaa la Katiba Tanzania (JUKATA), Bob Chacha Wangwe, amesema ni ajabu kuona kwamba amri zinazotolewa na mahakama zenye lengo la kusuluhisha migogoro kati ya wafugaji na hifadhi kutotekelezwa na Serikali.

“Ni jambo la kushangaza kwamba serikali inakuwa haiheshimu maamuzi yaliyotolewa na mahakama kuhusu utatuzi wa baadhi ya migogoro ya wafugaji na hifadhi. Inabidi Serikali itekelze maamuzi na amri zilizowahi kutolewa na mahakama kuhusu migogoro hiyo,” amesema Wangwe.

Awali, Kisabo aliitaka Serikali iingilie kati sakata la baadhi ya wafugaji katika Hifadhi ya Ngorongoro ambayo inadaiwa ng’ombe zao 1,000 zinadaiwa kupigwa mnada kinyume cha sheria, ili warudishiwe mifugo yao.

Kisabo aliitaka Mamlaka ya Hifadhi za Tanzania (TANAPA), iache kusumbua wananchi wa Ngorongoro ili kutekeleza amri ya mahakama iliyoelekeza wananchi hao wasiondolewe hifadhini hadi kesi ya msingi waliyofungua kupinga hatua ya Serikali kutenga baadhi ya ardhi zao kuwa pori la akiba.

Madai ya wafugaji kunyanyaswa yamekuwa yakitolewa mara kwa mara, lakini TANAPA imekuwa ikikanusha kwa madai kuwa mifugo inayochukuliwa ni ile iliyoingia hifadhini kinyume cha sheria.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Kesi ya mfanyakazi wa CRDB itaendelea J’tatu

Spread the love  MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kinondoni, Dar es Salaam inatarajia...

Habari Mchanganyiko

Mawasiliano Dar – Bagamoyo yarejea

Spread the loveMAWASILIANO ya barabara ya Mkoa wa Pwani na Dar es...

Habari Mchanganyiko

Tanesco: Mvua chanzo kukatika umeme leo

Spread the loveShirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limedai kuwa hitilafu iliyojitokeza katika...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Zara tours yajivunia kupandisha wageni 228 Mlima Kilimanjaro

Spread the loveKampuni ya utalii ya Zara tours ya mjini Moshi mkoani...

error: Content is protected !!