Monday , 11 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Wabunge waazimia kumchangia fedha, kumfariji Prof J
Habari za SiasaTangulizi

Wabunge waazimia kumchangia fedha, kumfariji Prof J

Spread the love

WABUNGE wamepitisha azimio la kumchangia fedha aliyekuwa Mbunge wa Mikumi (Chadema), Joseph Haule, ili kumfariji kutokana na matatizo ya kiafya aliyoyapata. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Azimio hilo limepitishwa leo tarehe 9 Novemba 2023, baada ya Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, wabunge kumuunga mkono katika uzinduzi wa taasisi yake ya Prof. Jay, aliyoanzisha kwa ajili ya kusaidia wagonjwa wa figo nchini, unaotarajiwa kufanyika tarehe 24 Novemba mwaka huu, jijini Dar es Salaam.

Baada ya Spika Tulia kutoa wito huo, Mbunge wa Nkasi Kaskazini (Chadema), Aidah Kenani, aliliomba mwongozo wa Spika Tulia kuhusu matatizo yaliyomkuta Prof. Jay, huku akipendekeza kila mbunge amchangie fedha kiasi cha Sh. 50,000.

Naye Mbunge wa Geita Vijijini (CCM), Joseph Kasheku maarufu kama Msukuma, alipendekeza kila mbunge amchangie Prof. Jay kiasi cha Sh. 200,000.

Kutokana na hoja hiyo kuungwa mkono na wabunge wengi, Spika Tulia alitoa mwongozo uliotaka wabunge kumchangia kulingana na uwezo wao kwa muda wa siku mbili, kuanzia leo Alhamisi hadi Ijumaa, kisha zoezi hilo likimalizika Prof. Jay akabidhiwe fedha zilizopatikana.

Kiongozi huyo wa Bunge, amesema pamoja na uzinduzi huo utakaofanyika tarehe 24 Novemba mwaka huu, pia litafanyika zoezi la kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia watu wenye matatizo ya figo.

Awali, Prof. Tulia wakati anaitambulisha taasisi ya Prof. Jay alisema “taasisi hii inatarajiwa kuzinduliwa katika Ukumbi wa Mlimani City, lengo lake pamoja na mambo mengine ni watanzania kuchangisha fedha kusaidia watu wenye changamoto za figo hapa nchini. “

“Mnakaribishwa kwa ajili ya kuungana na Prof. Jay kwenye jambo hili hasa tukizingatia alikuwa mbunge mwenzetu na alipata changamoto hii,” amesema SPika Tulia.

Prof. Jay ameanzisha taasisi hiyo baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na maradhi ya figo, ambaye kwa sasa anaendelea vizuri baada ya kupata matibabu ndani na nje ya nchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Biteko: Samia ni muumini wa maridhiano sio kwa kuigiza

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Mpango: Sitakufa bali nitaishi

Spread the loveMAKAMU  wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk....

Habari za SiasaTangulizi

Mbowe: Miaka 62 ya uhuru tujenge upya mioyo yetu

Spread the loveWAKATI Tanganyika ikiadhimisha miaka 62 tangu kupata uhuru, Mwenyekiti wa...

Habari za Siasa

Rais Samia asamehe wafungwa 2,244

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewasamehe wafungwa 2,244, huku akiwabadilishia...

error: Content is protected !!