Monday , 5 June 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Viongozi wa mashitaka Uganda wasitisha mgomo
Kimataifa

Viongozi wa mashitaka Uganda wasitisha mgomo

Yoweri Museven, Rais wa Uganda
Spread the love

VIONGOZI wa mashitaka nchini Uganda waliogoma wakidai  ongezeko la mishahara wamekubali ombi la serikali la kurejea kazini huku wakati madai yao yakishughulikiwa, anaandika Catherine Kayombo.

Serikali iliwaomba viongozi hao miezi mitatu kushughulikia madai yao, na kuwaomba kurejea kazini ili kuepusha msongamano wa kesi nchini humo ingawa ombi hilo lilikataliwa awali.

Msemaji Mkuu wa muungano wa viongozi wa mashtaka, Awali Kizito, aliiwaambia wanahabari kuwa mkutano mkuu ndiyo utakaoamua kusitisha ama kuendelea na mgomo huo.

“Hatima ya mgomo wetu ipo mikononi mwa mkutano mkuu wa wanachama wetu, tunatarajia kukutana  na kuamua ikiwa tutakubali ombi la serikali kusitisha mgomo huu au la”, alisema Kizito.

Viongozi hao  waliokuwa wamegoma kwa takribani wiki moja,  walikutana jana kuamua endapo wasitishe mgomo huo ambao umekwamisha kesi mahakamani.

Kufuatia mgomo huo, majaji wamekuwa wakiahirisha na kuchelewesha  kesi kwa ukosefu wa waendesha mashtaka.

Moja ya kesi zilizocheleweshwa nchini humo ni ya mauaji ya aliyekuwa msemaji wa polisi, Andrew Felix Kaweso.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Miili ya waliofariki kwenye ajali ya treni India, kukabidhiwa baada ya vipimo vya DNA

Spread the love  TAKRIBANI watu 260 wamefariki na wengine karibu 650 wamejeruhiwa...

Kimataifa

Kauli ya Rais wa China kuhusu ajira yawakatisha tamaa vijana

Spread the love  KAULI ya hivi karibuni ya Rais wa China, Xi...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Jeshi la Sudan lasitisha mazungumzo na wanamgambo wa RSF

Spread the love  JESHI rasmi la serikali ya Sudan, limesitisha ushiriki wake...

Kimataifa

Wakimbizi laki mbili wa Kongo, Burundi kuhemea chakula

Spread the love  SHIRIKA la Chakula la Umoja wa Mataifa (WFP), limetangaza...

error: Content is protected !!