Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Maseneta wamgomea Trump kuhusu Obama Care
Kimataifa

Maseneta wamgomea Trump kuhusu Obama Care

Spread the love

JUHUDI za rais wa Marekani, Donald Trump, kuubadilisha muswada wa afya wa Obamacare zinaelekea kugonga mwamba kufuatia baadhi ya viongozi katika chama cha Republican kutokukubaliana na mabadiliko hayo, anaandika Catherine Kayombo.

Kufuatia Trump kushindwa kupitisha muswada huo, tayari Maseneta wawili wa chama cha Republican wamepinga mpango wa chama chao  wa kuubadilisha muswada wa Obamacare hatua iliyofanya washindwe kupiga kura ya maoni.

Maseneta hao, Mike Lee na Jerry Morgan walitangaza kwamba hawawezi kuunga mkono mswaada huo, na kwamba  kukubaliana nao ni kuidhinisha sera mbaya katika nchi yao.

Mbali na hayo, Maseneta wengine wawili, Rand Paul na Susan Collins wametangaza kuupinga mswada huo wakidai kuwa hautoshi kufuta bima hiyo ya afya.

Mgawanyiko huu unajitokeza ambapo chama cha Republicans kinashikilia viti 52, katika Bunge la Seneti lenye wanachama  100, hali ambayo itakuwa vigumu kuidhinisha mswaada huo.

Maseneta kutoka chama cha Democratic wamesema kuwa hawatakubali kubadilisha mswaada huo wa Obamacare, lakini kwa kushirikiana na wanachama wa Republican wanaweza kufanya kazi kwa pamoja ili kuufanya uwe imara.

Rais Donald Trump, aliahidi kubadilisha muswada huo kama ahadi yake wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu, ikiwa ni namna mojawapo ya kubadilisha mfumo wa uongozi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!