Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Sirro abadilisha makamanda wa polisi
Habari Mchanganyiko

Sirro abadilisha makamanda wa polisi

Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Susan Kaganda, aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni
Spread the love

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro, amefanya mabadiliko ya makamanda wa polisi katika maeneo kadhaa, anaandika Catherine Kayombo.

Miongoni mwa waliobadilishwa vituo vya kazi ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Susan Kaganda, aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, ambaye amepelekwa kuwa Mkuu wa Kitengo cha Mafao na Fidia, makao makuu ya polisi.

Nafasi ya Kaganda imechukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Murilo Jumanne Murilo, aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga.

Aliyeteuliwa kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ni Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Simon Haule, aliyekuwa afisa mnadhimu wa Polisi Mkoa wa Mara.

Kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Polisi kwa vyombo vya habari, iliyosainiwa leo na Msemaji wa Polisi, Barnabas Mwakalukwa, mabadiliko hayo ni ya kawaida ndani ya jeshi hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

Habari Mchanganyiko

Makamba: China ni ya mfani kwa kupunguza umaskini

Spread the loveWAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, January...

error: Content is protected !!