Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Upinzani Zimbabwe walia rafu uchaguzi mkuu
Kimataifa

Upinzani Zimbabwe walia rafu uchaguzi mkuu

Spread the love

Kiongozi wa upinzani nchini Zimbabwe, Nelson Chamisa, ameituhumu serikali ya nchi hiyo kwa udanganyifu na wizi wa kura katika uchaguzi mkuu uliofanyika jana Jumatano. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Chamisa amewaambia waandishi habari mjini Harare, kuwa zoezi la kupiga kura lilighubikwa na vitendo vya udanganyifu na unyanyasaji kwa wapigakura, akigusia hitilafu kadhaa zilizojitokeza ikiwemo kuchelewa kufunguliwa kwa vituo vya uchaguzi.

Amesema chini ya robo ya vituo vyote vya kupigia kura kwenye mji mkuu Harare ndiyo vilifunguliwa kwa wakati.

Hata hivyo, taarifa iliyotolewa na Tume ya Uchaguzi iliyosema hali hiyo ilitokana na kuchelewa kwa uchapishaji karatasi za kupigia kura.

Upinzani umeilaumu serikali inayoongozwa na chama cha ZANU-PF, kinachoitawala nchi hiyo tangu uhuru mwaka 1980.

Kwenye uchaguzi huo ambao sasa matokeo yake yanasubiriwa, Rais Emmerson Mnangagwa wa ZANU-PF anayewania muhula mwingine madarakani dhidi ya Chamisa wa chama cha Citizens Coalition for Change (CCC).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Wadukuzi wa Kichana waiba barua pepe 60,000 za Serikali ya Marekani

Spread the loveWADUKUZI wa kichana wamedukua barua pepe 60000 serikali ya Marekani...

Kimataifa

Mahakama yamkuta na hatia Donald Trump

Spread the love  ALIYEKUWA Rais wa Marekani, Donald Trump, amekutwa na hatia...

Kimataifa

Harusi yageuka msiba 100 wakifariki kwa ajali ya moto

Spread the love  WATU takribani 100, akiwemo bibi na bwana harusi, wamefariki...

Kimataifa

Kampuni ya mali ya China Oceanwide yapata agizo la kufilisiwa huko Bermuda

Spread the love  MAHAKAMA ya Bermuda imetoa amri ya kufilisiwa kwa Kamapuni...

error: Content is protected !!