Kiongozi wa upinzani nchini Zimbabwe, Nelson Chamisa, ameituhumu serikali ya nchi hiyo kwa udanganyifu na wizi wa kura katika uchaguzi mkuu uliofanyika jana Jumatano. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Chamisa amewaambia waandishi habari mjini Harare, kuwa zoezi la kupiga kura lilighubikwa na vitendo vya udanganyifu na unyanyasaji kwa wapigakura, akigusia hitilafu kadhaa zilizojitokeza ikiwemo kuchelewa kufunguliwa kwa vituo vya uchaguzi.
Amesema chini ya robo ya vituo vyote vya kupigia kura kwenye mji mkuu Harare ndiyo vilifunguliwa kwa wakati.
Hata hivyo, taarifa iliyotolewa na Tume ya Uchaguzi iliyosema hali hiyo ilitokana na kuchelewa kwa uchapishaji karatasi za kupigia kura.
Upinzani umeilaumu serikali inayoongozwa na chama cha ZANU-PF, kinachoitawala nchi hiyo tangu uhuru mwaka 1980.
Kwenye uchaguzi huo ambao sasa matokeo yake yanasubiriwa, Rais Emmerson Mnangagwa wa ZANU-PF anayewania muhula mwingine madarakani dhidi ya Chamisa wa chama cha Citizens Coalition for Change (CCC).
Leave a comment