Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Upinzani Zimbabwe walia rafu uchaguzi mkuu
Kimataifa

Upinzani Zimbabwe walia rafu uchaguzi mkuu

Spread the love

Kiongozi wa upinzani nchini Zimbabwe, Nelson Chamisa, ameituhumu serikali ya nchi hiyo kwa udanganyifu na wizi wa kura katika uchaguzi mkuu uliofanyika jana Jumatano. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Chamisa amewaambia waandishi habari mjini Harare, kuwa zoezi la kupiga kura lilighubikwa na vitendo vya udanganyifu na unyanyasaji kwa wapigakura, akigusia hitilafu kadhaa zilizojitokeza ikiwemo kuchelewa kufunguliwa kwa vituo vya uchaguzi.

Amesema chini ya robo ya vituo vyote vya kupigia kura kwenye mji mkuu Harare ndiyo vilifunguliwa kwa wakati.

Hata hivyo, taarifa iliyotolewa na Tume ya Uchaguzi iliyosema hali hiyo ilitokana na kuchelewa kwa uchapishaji karatasi za kupigia kura.

Upinzani umeilaumu serikali inayoongozwa na chama cha ZANU-PF, kinachoitawala nchi hiyo tangu uhuru mwaka 1980.

Kwenye uchaguzi huo ambao sasa matokeo yake yanasubiriwa, Rais Emmerson Mnangagwa wa ZANU-PF anayewania muhula mwingine madarakani dhidi ya Chamisa wa chama cha Citizens Coalition for Change (CCC).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!