JESHI la Ukraine limedai kuua wanajeshi 5,840 wa Urusi tangu kuanza kwa vita kati ya nchi hizo mbili siku saba zilizopita. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 2 Machi, 2022 na Kamanda Mkuu wa Jeshi la Ukraine, Valeriy Zaluzhny kwa vyombo vya habari wakati akitoa takwimu mbalimbali za vita hiyo.
Kwa mujibu wa BBC, jumla ya hasara ambayo Ukraine imedai Urusi imepata katika vita hiyo ni pamoja na kupoteza wanajeshi 5,840, ndege 30, helkopta 31 na vifaru 211.
Pia Urusi imepoteza magari ya doria 862, vifaru vya 85 vyenye mfumo wa kutungua ndege, makombora 9, matenki 69 ya mafuta, magari 355 na mitambo 40 ya kurusha roketi.
Hata hivyo, madai hayajathibitishwa licha ya Waziri wa Ulinzi wa Uingereza, Ben Wallace kusema anaamini Majeshi ya Putin yamepata hasara kubwa wakati wa uvamizi wa Ukraine.
Leave a comment