Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ujerumani kuwalipa fidia wahanga wa ukoloni Tanzania, kurejesha mabaki
Habari za SiasaTangulizi

Ujerumani kuwalipa fidia wahanga wa ukoloni Tanzania, kurejesha mabaki

Spread the love

RAIS wa Shirikisho la Ujerumani, Dk. Frank Walter Steinmeier, ameahidi kufanya mazungumzo na watu walioathiriwa na ukoloni uliofanywa na taifa hilo, juu ya namna ya kuwafuta machozi, pamoja na kurejesha mabaki ya miili ya watu yaliyohifadhiwa katika makumbusho ya nchini kwao. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Rais Steinmeier ametoa ahadi hiyo leo tarehe 31 Oktoba 2023, Ikulu jijini Dar es Salaam, katika mkutano ulioandaliwa kwa ajili ya kutoa mrejesho wa masuala waliyojadili na kuafikiana na Rais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan.

“Tuweze kuangalia ukurasa mpya, ziara hii pia nimeiweka katika mrengo wa kuangalia yaliyotokea wakati wa ukoloni na kuonana na walioathiriwa na vita ya majimaji na pia nitakwenda kukutana na baadhi ya wahanga na nitaongea nao sababu najua walipitia kipindi kigumu. Yote watakayonieleza nitakwenda kuyarudisha Ujerumani,” amesema Rais Steinmeier.

Aidha, kiongozi huyo wa Ujerumani, amesema watafanya utafiti ili kujua athari zilizotokana na ukoloni.

“Tumejadiliana kuhusu namna gani ushirikiano uliopo utaweza kuendelezwa na tusisahau yaliyopita kati ya Ujerumani na Tanzania, kuna mambo tumepitia wakati wa ukoloni ni muhimu tuweze kukubaliana na tumefikia maamuzi kufanya utafiti wa ndani tuweze kuongeza maarifa katika hiki kilichotokea wakati wa ukoloni,” amesema Rais Steinmeier.

Awali, Rais Samia alisema katika mazungumzo yake na Rais Steinmeier, wamekubaliana kufungua majadiliano kuona jinsi ya kuzifuta machozi familia zilizoathiriwa wakati ilipokuwa inatawala Tanganyika.

“Kama mnavyojua Tanzania wakati ule Tanganyika, nadhani hata Zanzibar kwa muda mdogo tulikuwa chini ya utawala wa Ujerumani. Sasa katika utawala mambo mengi yamepita nimezungumza kwa urefu na tuko tayari kufungua majadiliano na kuona jinsi tutakavyoweza kukubaliana kwa yale yaliyopita Wakati wa utawala wa Ujerumani,” alisema Rais Samia na kuongeza:

“Vipi tufanye na najua kuna familia ambazo zinasubiri mabaki ya wapendwa wao ambayo yako kule makumbusho yaje yote. Tunakwenda kuzungumza na kuona vipi twende nayo vizuri.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!