Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Ujenzi shule ya kwanza kata ya Kilimani washika kasi
Elimu

Ujenzi shule ya kwanza kata ya Kilimani washika kasi

Spread the love

HATIMAYE kata ya Kilimani katika Jiji la Dodoma imeanza ujenzi wa shule ya msingi itakayogharimu kiasi cha Sh 80 milioni kwa kuanza na vyumba vinne vya madarasa. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Ujenzi huo wa shule ya msingi unatokana na kata hiyo kutokuwa na shule ya msingi wala  sekondari tangu kupatikana kwa Uhuru wa Tanganyika.


Hali hiyo inatajwa kusababisha watoto kutembea umbali wa kilomita tatu kusaka elimu katika vijiji jirani.

Hata hivyo, leo tarehe 11 Oktoba 2023 Viongozi wa Kamati ya siasa ya  Chama Cha Mapinduzi Kata ya Kilimani Jijini Dodoma pamoja na Wajumbe wa  Sekretarieti   ya kata ya kilimani wamefanya ziara ya kukagua mradi wa ujenzi wa Shule  ya Msingi  unaotekelezwa katika Mtaa wa Chinyoyo.

Pamoja na kasi ya ujenzi huo  unaoendelea  viongozi hao wamesisitiza kasi katika ujenzi huo ili ukamilike kwa haraka na kwa wakati.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi kata ya kilimani, Nathani Chibeye amesema ujenzi huo wa shule ya msingi utakuwa mkombozi kwa kata ya kilimani na kuondoa adha ya watoto kutembea umbali mrefu kwenda shule za jirani.

Kwa upande wake Katibu wa CCM kata ya Kilimani, Rotta Ndimbo ameitaka kamati ya ujenzi na mkandarasi kuhakikisha wanatanguliza uzalendo katika ujenzi wa shule hiyo ili thamani ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya ujenzi huo zitumike kama zilivyo kusudiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

error: Content is protected !!