Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ugonjwa wa shahidi wakwamisha kesi ya kina Mdee, Chadema
Habari za Siasa

Ugonjwa wa shahidi wakwamisha kesi ya kina Mdee, Chadema

Spread the love

MAHAKAMA Kuu, Masjala Kuu ya Dar es Salaam, imeahirisha usikilizwaji wa kesi iliyofunguliwa na wabunge viti maalum 19, kupinga kufukuzwa Chadema, kutokana na shahidi aliyetarajiwa kuendelea kuhojiwa na upande wa wajibu maombi, Hawa Mwaifunga, kuumwa mgongo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kesi hiyo Na. 36/2022, iliyotarajiwa kuendelea kusikilizwa leo Ijuma, tarehe 21 Oktoba 2022, imeahirishwa na mahakama  mbele ya Jaji Cyprian Mkeha, baada ya Mwaifunga kupitia mawakili wake, kuomba ahirisho akidai anaumwa mgongo.

Mwaifunga kupitia mawakili wake, aliwasilisha madai ya kuugua, katika kikao cha majadiliano mafupi kati ya Jaji Mkeha na mawakili wa waleta maombi na wajibu maombi,ambapo Jaji Mkeha aliahirisha kesi hadi tarehe 3 Novemba mwaka huu.

Mawakili wanaomuwakilisha Mwaifunga na wenzake 18 katika kesi hiyo ni, Emmanuel Ukashu, Ipilinga Panga, Edson Kilatu na Aliko Mwamanenge.

Wakili wa Chadema, wakiongozwa na Peter Kibatala (katikati) wakiwa mahakamani

Siku hiyo, Mwaifunga ataendelea kuulizwa maswali ya dodoso kuhusu malalamiko yake aliyoyaweka kwenye hati yake ya kiapo na hati ya kiapo cha pamoja na mawakili wa mjibu maombi wa kwanza, Bodi ya Wadhamini ya Chadema.

Mbunge huyo ambaye alikuwa Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la Chadema (BAWACHA), alianza kuhojiwa maswali hayo na Kiongozi wa Jopo la Mawakili wa Chadema, Peter Kibatala, tarehe 13 Oktoba 2022, baada ya mbunge mwenzake, Grace Tendega kumaliza kuhojiwa maswali hayo.

Aidha, Jaji Mkeha amepanga tarehe nyingine za kusikilizwa kesi hiyo kuwa ni 4,5,8,9 Novemba 2022 na tarehe 6, 7 Desemba mwaka huu.

Katika tarehe hizo, mawakili wa Chadema wataendelea kuwahoji wabunge sita waliobakia, kati ya nane waliyoruhusiwa na mahakama hiyo kuwahoji ili watoe ushahidi wao kuhusu hati zao za viapo.

Wabunge hao sita walioitwa kuhojiwa na Chadema ni, Ester Bulaya, Nusrat Hanje, Jesca Kishoa, Esther Matiko, Cecilia Pareso na Halima Mdee.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!