Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Twibhoki, Graiyaki zafungiwa, Mother of Mercy, St. Marys’ Mbezi Beach zapewa onyo
ElimuTangulizi

Twibhoki, Graiyaki zafungiwa, Mother of Mercy, St. Marys’ Mbezi Beach zapewa onyo

Spread the love

BARAZA la Mitihani la Tanzania limefungia vituo vya mtihani viwili ambavyo ni Twibhoki (PS0904095) na Graiyaki (PS0904122) vyote vya Halmashauri ya Serengeti mkoa wa Mara vilivyothibitika kupanga kufanya udanganyifu katika Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi (PSLE) 2023.  Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Katibu Mtendaji wa NECTA, Dk. Said Mohamed amesema hatua hiyo imechukuliwa kwa mujibu wa Kifungu 4(8) cha Kanuni za Mitihani mwaka 2016 mpaka hapo Baraza litakapojiridhisha kuwa ni salama kwa uendeshaji wa Mitihani ya Taifa.

 

NECTA, Dk. Said Mohamed

Aidha, baraza hilo pia limeziandikia barua za onyo vituo vya mtihani vinne ambavyo ni Mother of Mercy (PS0203133), St. Marys’ Mbezi Beach (PS0203088) vya Halmashauri ya Kinondoni mkoa wa Dar es Salaam, Charm Modern (PS0103111) cha Halmashauri ya Karatu mkoa wa Arusha pamoja na Morotonga (PS0904042) cha Halmashauri ya Serengeti mkoa wa Mara.

Amesema vituo hivyo vilijaribu kujihusisha na vitendo vya udanganyifu katika mtihani.

“Vituo hivyo vitakuwa chini ya uangalizi wa Baraza la Mitihani mpaka hapo Baraza litakapojiridhisha kuwa ni vituo salama kwa uendeshaji wa Mitihani ya Taifa,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

Habari MchanganyikoTangulizi

Walimu 5000 Songwe waililia CWT kuwanyima sare

Spread the loveZaidi ya walimu 5000 ambao ni wanachama wa Chama cha...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!