Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Trump kujisalimisha kesi ya kubatilisha uchaguzi
Kimataifa

Trump kujisalimisha kesi ya kubatilisha uchaguzi

Donald Trump
Spread the love

RAIS wa zamani wa Marekani, Donald Trump amesema kuwa atajisalimisha mwenyewe jimboni Georgia Alhamis wiki hii ili kukabiliana na mashtaka ya udanganyifu na makosa yanayohusu tuhuma za kutaka kubatilisha matokeo ya uchaguzi. Anaripoti Maryam Mudhihir kwa msaada wa mitandao ya kimataifa…(endelea.)

Kupitia mtandao wake wa kijamii wa Truth Social siku ya jana Jumatatu, Trump alisema kwamba siku hiyo ya Alhamis atakamatwa na Mwanasheria mwenye misimamo mikali, Fani Wills, ambaye alifungua mashtaka ya manne mwaka huu dhidi yake.

Jaji katika kesi hiyo, awali aliidhinisha dhamana ya Dola za Kimarekani 200,000 kwa Trump katika kesi hiyo ya udanganyifu iliyofunguliwa dhidi yake katika jimboh hilo la kusini.

Trump na washitakiwa wengine 18 katika kesi hiyo ya kihistoria watakuwa na muda wa mwisho wa hadi saa sita mchana siku ya Ijumaa kujisalimisha wenyewe katika mamlaka za Georgia.

Kwenye ujumbe wake kupitia Truth Social, Trump amedai kwamba mwanasheria Wills anashirikiana na wizara ya sheria ‘kihuni’.

Trump anadai kuwa mashtaka yote dhidi yake yamesukwa ili kuzuia jaribio lake la kuwania muhula wa pili wa urais wakati akiongoza ndani ya chama chake cha Republican.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!