RAIS wa zamani wa Marekani, Donald Trump amesema kuwa atajisalimisha mwenyewe jimboni Georgia Alhamis wiki hii ili kukabiliana na mashtaka ya udanganyifu na makosa yanayohusu tuhuma za kutaka kubatilisha matokeo ya uchaguzi. Anaripoti Maryam Mudhihir kwa msaada wa mitandao ya kimataifa…(endelea.)
Kupitia mtandao wake wa kijamii wa Truth Social siku ya jana Jumatatu, Trump alisema kwamba siku hiyo ya Alhamis atakamatwa na Mwanasheria mwenye misimamo mikali, Fani Wills, ambaye alifungua mashtaka ya manne mwaka huu dhidi yake.
Jaji katika kesi hiyo, awali aliidhinisha dhamana ya Dola za Kimarekani 200,000 kwa Trump katika kesi hiyo ya udanganyifu iliyofunguliwa dhidi yake katika jimboh hilo la kusini.
Trump na washitakiwa wengine 18 katika kesi hiyo ya kihistoria watakuwa na muda wa mwisho wa hadi saa sita mchana siku ya Ijumaa kujisalimisha wenyewe katika mamlaka za Georgia.
Kwenye ujumbe wake kupitia Truth Social, Trump amedai kwamba mwanasheria Wills anashirikiana na wizara ya sheria ‘kihuni’.
Trump anadai kuwa mashtaka yote dhidi yake yamesukwa ili kuzuia jaribio lake la kuwania muhula wa pili wa urais wakati akiongoza ndani ya chama chake cha Republican.
Leave a comment