Monday , 13 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Telegram kudhibiti Magaidi Indonesia
Kimataifa

Telegram kudhibiti Magaidi Indonesia

Mtandao wa Telegram
Spread the love

MTANDAO wa kijamii wa Telegram, umeahidi kuwa utafunga akaunti zinazohusiana na ugaidi nchini Indonesia, anaandika Hamisi Mguta.

Maamuzi hayo ni kufuatia Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia nchini humo kufunga huduma za mtandao huo nchini humo siku ya Ijumaa kwa kudai kuwa Telegram imetumiwa kuunga mkono itikadi kali na kutoa maelekezo ya kufanya mashambulizi.

Taarifa kupitia BBC zinaeleza kuwa Pavel Durov, Mwanzilishi wa mtandao huo kupitia taarifa yake amesema kuwa Telegram sasa imeondoa akaunti zote zinazohusika na ugaidi zilizotajwa na serikali.

Pavel Durov, Mwanzilishi wa Mtandao wa Telegram

Hatua hiyo inakuja huku kukiwa na wasiwasi wa kuibuka kwa kundi la Islamic State kusini mashariki mwa Asia ambalo limedai kuhusika kwenye mashambulizi kadhaa nchini Indonesia mwaka huu na limepigana na jeshi mjini Marawi katika kisiwa cha mindanao nchini Ufilipino.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

error: Content is protected !!