Thursday , 23 March 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Telegram kudhibiti Magaidi Indonesia
Kimataifa

Telegram kudhibiti Magaidi Indonesia

Mtandao wa Telegram
Spread the love

MTANDAO wa kijamii wa Telegram, umeahidi kuwa utafunga akaunti zinazohusiana na ugaidi nchini Indonesia, anaandika Hamisi Mguta.

Maamuzi hayo ni kufuatia Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia nchini humo kufunga huduma za mtandao huo nchini humo siku ya Ijumaa kwa kudai kuwa Telegram imetumiwa kuunga mkono itikadi kali na kutoa maelekezo ya kufanya mashambulizi.

Taarifa kupitia BBC zinaeleza kuwa Pavel Durov, Mwanzilishi wa mtandao huo kupitia taarifa yake amesema kuwa Telegram sasa imeondoa akaunti zote zinazohusika na ugaidi zilizotajwa na serikali.

Pavel Durov, Mwanzilishi wa Mtandao wa Telegram

Hatua hiyo inakuja huku kukiwa na wasiwasi wa kuibuka kwa kundi la Islamic State kusini mashariki mwa Asia ambalo limedai kuhusika kwenye mashambulizi kadhaa nchini Indonesia mwaka huu na limepigana na jeshi mjini Marawi katika kisiwa cha mindanao nchini Ufilipino.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Raila Odinga: Tutafanya maandamano makubwa mara mbili kwa wiki

Spread the love KIONGOZI wa upinzani nchini Kenya, Raila Amollo Odinga ametangaza...

Kimataifa

Magharibi kuwekeza silaha Indo-Pacific, China yachochea

Spread the love KUVUNJIKA ushirhikiano wa China na Magharibi uliodumu kwa takribani...

Kimataifa

Ruto amlaumu Odinga kujaribu kuanzisha mgogoro kwa mara ya pili

Spread the love  RAIS wa Kenya William Ruto amesema kwamba hatakubali “kutoijali...

Kimataifa

Putin, Xi Jinping kujadili mpango kumaliza vita nchini Ukraine

Spread the love  Vladimir Putin amesema atajadili mpango wenye vipengele 12 wa...

error: Content is protected !!