Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Tanzania, Kenya, Ethiopia, Nigeria zapigwa ‘Stop’ kuingia UAE kisa Corona
AfyaKimataifa

Tanzania, Kenya, Ethiopia, Nigeria zapigwa ‘Stop’ kuingia UAE kisa Corona

Spread the love

 

UMOJA wa Falme za Kiarabu (UAE), zimesitisha safari za ndege kwa abiria wanaotoka nchi za Tanzania, Kenya, Ethiopia na Nigeria, huku ikiongeza vikwazo vya usafiri kwa abira wa Uganda na Ghana. Unaripoti Mtandao wa BBC Swahili … (endelea).

Kwa mujibu wa mtandao huo, agizo hilo litaanza kutekelezwa usiku wa tarehe 25 Desemba 2021, ambapo chanzo cha sitisho la safari za ndege kwa nchi hizo, kikitajwa ni kudhibiti usambaaji wa Ugonjwa wa Virusi vya Corona (UVIKO-19-19).

Marufuku hiyo ilitolewa jana Alhamisi, tarehe 23 Desemba 2021 na Mamlaka ya Kudhibiti Dharura na Majanga UAE (NCEMA) na Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini humo (GCAA).

Kwa mujibu wa mitandao ya kimataifa, watu watakaoruhusiwa kuingia katika umoja huo ni, raia wake, wanadiplomasia na wajumbe maalum kati ya nchi hizo na UAE.

Watu hao walioruhusiwa kuingia UAE wamepewa masharti kadhaa, ikiwemo kuwasilisha majibu ya vipimo yanayoonesha hawana UVIKO-19, vipimo hivyo vifanyike ndani ya saa 48.

Pamoja na kupimwa tena wakiwa katika uwanja wa ndege, ndani ya saa sita kabla ya safari kuanza.

Hata hivyo, safari za ndege kutoka UAE kwenda katika mataifa hayo zitaendelea kama kawaida.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

error: Content is protected !!