Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo Mmewasikia KMC, wataka kuwapa mashabiki wao zawadi ya Krisimasi
Michezo

Mmewasikia KMC, wataka kuwapa mashabiki wao zawadi ya Krisimasi

Spread the love

 

KLABU ya KMC ya Kinondoni inayoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara, imetamba kuibuka na ushindi kwenye mchezo wa leo wa Ligi Kuu dhidi ya Simba, ili iwe kama sehemu ya zawadi ya sikukuu ya Krisimasi kwa mashabiki wa timu hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo wa duru la kwanza wa Ligi Kuu Tanzania bara utapigwa hii leo majira ya saa 10 kamili jioni kwenye dimba la Ali Hassan Mwinyi, mkoani Tabora.

Akizungumza na Raia Mwema kuelekea mchezo huo Afisa Habari wa KMC, Christina Mwangala amejitanabaisha kuwa mchezo huo utakuwa mgumu lakini pia mwepesi kutokana na walivyojiandaa na wanataka kutumia matokeo ya mchezo huo kama zawadi ya sikukuu ya Krisimasi kwa mashabiki wa timu yao.  

“Mchezo wa kesho ni mguu lakini mwepesi, ni mechi ambazo wachezaji wamezizoea na kila mmoja anajiandaa kwa namna yake, ni mechi nzuri na kuvutia tunahitaji kuwapa mashabiki wetu zawadi ya Christmas na mwaka mpya,” alisema Afisa habari huyo.

Kikosi hiko kinaingia kwenye mchezo huo, huku kikiwa na kumbukumbu ya kutoka sare ya bila kufungana kwenye mchezo uliopita dhidi ya Mtibwa Sugar uliopigwa kwenye Uwanja wa Manungu, Turiani mkoani Morogoro.

Katika michezo mitano iliyopita ya Ligi Kuu Tanzania Bara, KMC haijapoteza mchezo hata mmoja na kushinda michezo mitatu, huku ikienda sare mara mbili.

Kikosi cha Simba kikifanya mazoezi

Aidha msemaji huyo aliendelea kusema kuwa mpaka sasa kikosi chao hakuna changamoto yoyote ya maradhi yaliyoibuka hivi karibuni.

“Kwetu sisi changamoto tulipitia kwenye mechi zaidi ya Mtibwa Sugar, lakini hatukuweka wazi na wachezaji waliweza kukava na tukacheza mechi na Mtibwa lakini mpaka sasa hakuna anayeumwa,” alisema Afisa Habari huyo.

Kikosi cha Kmc kiliwasili mkoani Tabora siku ya jana na kufanya maandalizi ya mwisho kuwakabili mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!