Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Sunak,Truss waanza kuchuana kumrithi Johnson uongozi Conservative
Kimataifa

Sunak,Truss waanza kuchuana kumrithi Johnson uongozi Conservative

Spread the love

 

WAGOMBEA  wawili katika kinyang’anyiro cha uongozi wa chama cha Conservative leadership wamewasilisha mipango yao kwa wajumbe wa chama ambao watamchagua mrithi wa Boris Johnson. Yanaripoti Mashirika ya Kimataifa.

Kwa mujibu wa BBC, Rishi Sunak na Liz Truss walipata kura nyingi zaidi katika uchaguzi wa mwisho wa wabunge Jumatano.

Akiandika katika gazeti la Daily Telegraph, Sunak amesema atapanga “mageuzi makubwa kama yale ambayo Margaret Thatcher aliyafanya katika miaka ya 1980”.

Katika Daily Mail, Truss ameahidi “kukata kodi, kuboresha biashara, na kuweka sera rafiki za biashara za Conservative”.

Wawili hao waliibuka kuwa wagombea wakuu baada ya Truss kubadilisha ushindi mdogo wa Waziri wa biashara Penny Mordaunt, ambaye wakati mmoja alipendelewa, kwa kupata uungaji mkono wa Waconsertvative 113 dhidi ya Mordaunt aliyepata 105.

Kansela wa zamani Sunak, ambaye aliendelea kuongoza miongoni mwa wabunge, alishinda kwa kura 137.

Kura za maoni zinaonyesha kuwa ni mtu ambaye ana umaarufu wa kiwango cha chini zaidi miongoni mwa wajumbe wa chama cha Conservative ambao watapiga kura kwa mgombea ajaye mwezi ujao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!