SPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, amesema kengele ya hatari iliyofanya mhimili huo usitishe shughuli zake kwa muda, imetokana na marekebisho yaliyokuwa yanafanywa katika sehemu ya chimi ya ukumbi wake, yaliyosababisha vumbi na kupelekea mifumo ya usalama kuhisi kuna moshi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).
Spika Tulia ametoa taarifa hiyo leo Jumanne, muda mfupi baada ya kikao cha Bunge kurejea.
“Hitilafu imetokana na kwamba walikuwa wanafanya marekebisho ilidi watindue eneo, katika kutindua vumbi ikatoka na vinavyonasa hitilafu ikanasa ile vumbi kama moshi. Kwa hiyo ndiyo maana ikapiga kelele kuashiria kuna shida kwenye jengo hili,” amesema Spika Tulia.
Spika Tulia amewatoa hofu wabunge na wananchi kwamba changamoto hiyo imedhibitiwa na kwamba marekebisho yanaendelea kwa utaratibu mzuri.
Kengele ya dharura ililia wakati Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya, anajibu maswali ya wabunge. Ambapo Spika Tulia aliahirisha kikao hicho kwa muda na kuwataka wbaunge watoke nje ya ukumbi.
Leave a comment