KLABU ya Soka ya Simba SC. imemtimua Kocha Mkuu wa kikosi cha timu hiyo, Zoran Maki baada ya kufikia makubaliano ya pande zote mbili ya kuvunja mkataba. Anaripoti Felister Mwaipeta, TUDARCo … (endelea).
Pia imefikia makubaliano ya kusitisha mikataba ya Kocha wa viungo, Sbai Karim na Kocha wa Makipa Mohamed Rachid.
Taarifa iliyotolewa leo tarehe 6 Septemba, 2022 na Afisa mtendaji Mkuu wa timu hiyo, Barbara Gonzalez imeeleza kuwa uongozi wa klabu hiyo unawashukuru makocha hao kwa mchango wao ndani ya klabu yetu na inawatakia kila heri katika majukumu yao mapya.
“Kuelekea mchezo wetu wa kesho dhidi ya KMC kikosi chetu kitakuwa chini ya Kocha msaidizi, Selemani Matola.
“Tayari mchakato wa haraka wa kutafuta makocha wapya umeanza na unatarajiwa kukamilika hivi punde,” imesema taarifa hiyo.
Leave a comment