Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Shinyanga yajipanga utekelezaji kampeni msaada kisheria ya Mama Samia
Habari Mchanganyiko

Shinyanga yajipanga utekelezaji kampeni msaada kisheria ya Mama Samia

Spread the love

MKOA wa Shinyanga umeahidi kushirikiana na Wizara ya Katiba na Sheria pamoja na Shirika la Legal Services Facility (LSF), katika utekelezaji wa kampeni ya kitaifa ya msaada wa kisheria ya Mama Samia. Anaripoti Mwandishi Wetu, Shinyanga…(endelea).

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Christina Mndeme akitoa hotuba ya ufunguzi wakati wa uzinduzi rasmi wa utekelezaji kampeni ya kitaifa ya huduma ya msaada wa kisheria ya Mama Samia Mkoani Shinyanga.


Ahadi hiyo ilitolewa jana Jumapili na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Christina Mndeme, katika uzinduzi wa kampeni hiyo inayofahamika kwa jina la Mama Samia Legal Aid Campaign, mkoani humo.

Mndeme ameagiza watendaji na viongozi wa kata za Shinyanga kutenga maeneo yatakayotumiwa na watoa msaada wa kisheria wakati wa utekelezaji wa kampeni hiyo hasa maeneo ya pembezoni.

Meneja Rasilimali na Mawasiliano LSF, Jane Matinde akizungumza kwa niaba ya Makamu Mwenyekiti wa kampeni ambaye Mkurugenzi Mtendaji wa Legal Services Facility (LSF), Lulu Ng’wanakilala wakati wa uzinduzi rasmi wa utekelezaji kampeni ya kitaifa ya huduma ya msaada wa kisheria ya Mama Samia Mkoani Shinyanga.


Kampeni ya Mama Samia Legal Aid, inatarajiwa kufanyia Shinyanga kuanzia tarehe 11 hadi 21 Juni 2023.

“Kwa mara nyingine tena, ninatoa wito kwamba sisi sote tushikamane katika kumuunga mkono Kiongozi wetu, Dk. Samia Suluhu Hassani,  katika kuondoa kadhia na viashiria vyote vya kuminya upatikanaji wa haki hususan ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto ambayo ndiyo changamoto kubwa ya Mkoa wa Shinyanga,” alisema  Mndeme.

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Pauline Gekul, alisema Serikali kwa kushirikiana na wadau wengine imedhamiria kuhakikisha kampeni hiyo inawafikia wananchi wote wa Tanzania Bara na Zanzibar.

Alisema kampeni hiyo inalenga kuunga mkono juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan, katika kuimarisha haki za binadamu na utawala Bora.

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Pauline Gekul akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa utekelezaji kampeni ya kitaifa ya huduma ya msaada wa kisheria ya Mama Samia Mkoani Shinyanga.

“Huduma ya msaada wa kisheria kuwafikia wananchi bure ni mapenzi na upendo mkubwa wa Rais Samia  kwa mwananchi wa hali ya chini,” alisema  Gekul.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Marry Makondo, alisema kampeni hiyo itasaidia kushighilikia masuala yote ya ukatili wa kijinsia, migogoro ya ardhi, mirathi na wosia, pamoja na kuelimisha Jamii kuhusu haki na wajibu wao kisheria na kikatiba.

Meneja Rasilimali na Mawasiliano kutoka LSF, Jane Matinde, alisema  uzinduzi huo unakwenda kufanyika kila mkoa, huku ukienda sambamba na utoaji wa huuduma

za msaada wa kisheria ili kuchochea upatikanaji wa haki kwa wananchi hasa wasiojiweza ikiwemo wanawake, watoto na makundi maalum.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

error: Content is protected !!