Thursday , 30 March 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Sheikh apigwa risasi, auawa
Kimataifa

Sheikh apigwa risasi, auawa

Sheikh Ali Amini
Spread the love

 

SHEIKH Ali Amini, Imamu mashuhuri Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), amepigwa risasi na kuuawa hapo hapo wakati akiswalisha swala ya Magharibi, mjini Beni. Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Taarifa zinaeleza, mtu mwenye silaha, alimfyatulia risasi Sheikh Ali wakati wa swala ya Magharibi juzi Jumamosi, tarehe 1 Mei 2021, baada ya kufanya tukio hilo, alikimbia.

Mashariki mwa Congo imekumbwa na hali mbaya ya usalama, ikiwemo mashambulizi yanayodaiwa kutekelezwa na kundi la IS.

Makundi mengi yenye silaha yanayoendesha operesheni zao nchini humo, yametokana na mizozo iliyokumba nchi hiyo miaka ya 1990.

Kifo cha Sheikh Ali, kimesababisha mshtuko mkubwa katika mji huo wenye wakazi wapatao 200,000.

Mwanaharakati wa haki za binadamu mjini humo, Stewart Muhindo, amesema tukio hili ni la kwanza kutokea mjini humo.

”Ilitokea wakati wa swala ya Magharibi. Risasi zilifyatuliwa ndani ya msikiti na kumpata Imam. Mtu huyo alitoka eneo la tukio, alikuwa na mwenzake ambaye alikuwa akimsubiri na pikipiki,” Mwanaharakati Muhindo.

Kundi linalohusiana na IS katika eneo hilo liitwalo Kundi la Waasi la Kiislamu (ADF), linahusishwa na mauaji hayo.

ADF iliundwa zaidi ya miaka 20 iliyopita katika nchi jirani ya Uganda, kwa lengo la kupambana na madai ya ubaguzi dhidi ya Waislamu. Lilifurushwa na jeshi la Uganda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Nyumba ya babu yake Makamu wa Rais wa Marekani yatafutwa Zambia

Spread the love  KAMALA Harris, makamu wa rais wa Marekani, amepanga kutembelea...

Kimataifa

Benki ya Uswizi mbioni kuziwekea vikwazo akaunti za siri za Wachina

Spread the love  WAKATI Serikali na Benki ya Uswizi ikichukua hatua kali...

Kimataifa

Netanyau asitisha mipango yenye utata marekebisho mfumo wa sheria

Spread the love  WAZIRI Mkuu wa nchini Israel, Benjamin Netanyahu amesema atachelewesha...

Kimataifa

Raila ahutubia waandamanaji, mabomu yarindima

Spread the loveMSAFARA wa kiongozi wa Azimio la Umoja-One Kenya, Raila Odinga...

error: Content is protected !!