Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Sheikh apigwa risasi, auawa
Kimataifa

Sheikh apigwa risasi, auawa

Sheikh Ali Amini
Spread the love

 

SHEIKH Ali Amini, Imamu mashuhuri Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), amepigwa risasi na kuuawa hapo hapo wakati akiswalisha swala ya Magharibi, mjini Beni. Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Taarifa zinaeleza, mtu mwenye silaha, alimfyatulia risasi Sheikh Ali wakati wa swala ya Magharibi juzi Jumamosi, tarehe 1 Mei 2021, baada ya kufanya tukio hilo, alikimbia.

Mashariki mwa Congo imekumbwa na hali mbaya ya usalama, ikiwemo mashambulizi yanayodaiwa kutekelezwa na kundi la IS.

Makundi mengi yenye silaha yanayoendesha operesheni zao nchini humo, yametokana na mizozo iliyokumba nchi hiyo miaka ya 1990.

Kifo cha Sheikh Ali, kimesababisha mshtuko mkubwa katika mji huo wenye wakazi wapatao 200,000.

Mwanaharakati wa haki za binadamu mjini humo, Stewart Muhindo, amesema tukio hili ni la kwanza kutokea mjini humo.

”Ilitokea wakati wa swala ya Magharibi. Risasi zilifyatuliwa ndani ya msikiti na kumpata Imam. Mtu huyo alitoka eneo la tukio, alikuwa na mwenzake ambaye alikuwa akimsubiri na pikipiki,” Mwanaharakati Muhindo.

Kundi linalohusiana na IS katika eneo hilo liitwalo Kundi la Waasi la Kiislamu (ADF), linahusishwa na mauaji hayo.

ADF iliundwa zaidi ya miaka 20 iliyopita katika nchi jirani ya Uganda, kwa lengo la kupambana na madai ya ubaguzi dhidi ya Waislamu. Lilifurushwa na jeshi la Uganda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!