Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Sakata la uhamiaji Rwanda lamng’oa waziri Uingereza
Kimataifa

Sakata la uhamiaji Rwanda lamng’oa waziri Uingereza

Spread the love

Waziri wa Uhamiaji wa Uingereza, Robert Jenrick amejiuzulu baada ya serikali ya nchi hiyo kuchapisha sheria kuhusu mkataba wenye utata na Rwanda wa kutuma wahamiaji katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Waziri wa Mambo ya Ndani, James Cleverly aliwaambia wabunge jana Jumatano kwamba Robert Jenrick amejiuzulu kwa madai kuwa sheria hiyo ya dharura haijitoshelezi.

“ Sikubaliani na sheria inayopendekezwa kwa sasa kupitia Bunge, kwani siamini kwamba inatupa fursa nzuri zaidi ya kufanikiwa,” ameandika waziri huyo katika barua aliyoielekeza kwa Waziri Mkuu wa Uingereza, Rishi Sunak.

Mapema Jumatano Rwanda ilionya kujiondoa katika mkataba wa kuwapokea wahamiaji iwapo Uingereza haitaheshimu sheria za kimataifa.

Uingereza na Rwanda zilitia saini mkataba mpya Jumanne katika jitihada za kufufua pendekezo linaloonekana kuwa na utata la Uingereza la kuwahamisha wahamiaji katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki, pendekezo ambalo awali lilipingwa na mahakama ya Uingereza.

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uingereza James Cleverly na Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda Vincent Biruta walitia saini makubaliano hayo mjini Kigali nchini Rwanda.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda, Vincent Biruta, ambaye alitia saini mkataba huo wa pande mbili, alisema ukiukaji wowote wa mikataba ya kimataifa unaweza kuifanya Rwanda kujiondoa katika mkataba huo.

Mpango wa Rwanda ni sehemu ya mkakati wa kupunguza idadi ya watu wanaoingia nchini Uingereza kwa kuvuka bahari kwa boti.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!