Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Safari za mabasi usiku zapigwa ‘stop’
Habari Mchanganyiko

Safari za mabasi usiku zapigwa ‘stop’

Spread the love

JESHI la Polisi limetangaza kusitisha safari za usiku kwa baadhi ya magari ya abiria yanayokwenda mikoani. Anaripoti Hamis Mguta…(endelea).

CP Liberatus Sabas, Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa jeshi hilo amesema, wameamua kuchukua hatua hiyo kutokana na sababu za kiusalama na kuwa, mabasi yatakayoruhusiwa kufanya safari zake za usiku ni  Morogoro -Dar es Salaam, Shinyanga – Mwanza pekee.

Amesema, mabasi ambayo hayataruhusiwa kufanya safari zake usiku ni Dar es Salaam-Kahama-Mwanza, Dar es Salaam-Tabora-Katavi, Kahama- Geita-Kagera, Kahama kwenda mikoa mingine iliyopo mipakani pamoja na Dar es Salaam-Tabora kwenda katika wilaya zake.

“Jeshi la Polisi limejipanga kikamilifu kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama, kulifanyia kazi suala la usalama na baadaye mabasi yote yataruhusiwa kutembea usiku,” amesema.

Kwa mujibu wa CP Sabas ni kwamba, zoezi la kuzuia mabasi hayo kusafiri usiku limeanza kutekelezwa kabla ya taarifa hizo kutolewa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

error: Content is protected !!