Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Safari za mabasi usiku zapigwa ‘stop’
Habari Mchanganyiko

Safari za mabasi usiku zapigwa ‘stop’

Spread the love

JESHI la Polisi limetangaza kusitisha safari za usiku kwa baadhi ya magari ya abiria yanayokwenda mikoani. Anaripoti Hamis Mguta…(endelea).

CP Liberatus Sabas, Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa jeshi hilo amesema, wameamua kuchukua hatua hiyo kutokana na sababu za kiusalama na kuwa, mabasi yatakayoruhusiwa kufanya safari zake za usiku ni  Morogoro -Dar es Salaam, Shinyanga – Mwanza pekee.

Amesema, mabasi ambayo hayataruhusiwa kufanya safari zake usiku ni Dar es Salaam-Kahama-Mwanza, Dar es Salaam-Tabora-Katavi, Kahama- Geita-Kagera, Kahama kwenda mikoa mingine iliyopo mipakani pamoja na Dar es Salaam-Tabora kwenda katika wilaya zake.

“Jeshi la Polisi limejipanga kikamilifu kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama, kulifanyia kazi suala la usalama na baadaye mabasi yote yataruhusiwa kutembea usiku,” amesema.

Kwa mujibu wa CP Sabas ni kwamba, zoezi la kuzuia mabasi hayo kusafiri usiku limeanza kutekelezwa kabla ya taarifa hizo kutolewa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

Habari Mchanganyiko

Somo la dini: Waislamu waishukia Serikali, wizara yatoa kauli

Spread the loveJUMUIYA na Taasisi za Kiislamu Tanzania, imetupia lawama Serikali ikidai...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!