Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais wa Somalia amtimua waziri mkuu wake akimtuhumu kutaka kumpinuda
Kimataifa

Rais wa Somalia amtimua waziri mkuu wake akimtuhumu kutaka kumpinuda

Spread the love

 

RAIS wa Somalia, anayemaliza muda wake, Mohamed Abdullahi Farmajo, amemsimamisha kazi Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Mohamed Hussein Roble, ili kupisha uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazomkabili za ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa jana Jumapili, tarehe 26 Desemba 2021 na Ofisi ya Rais wa Somalia.

Kwa mujibu wa mitandao ya kimataifa, Roble anatuhumiwa kupanga mapinduzi yasiyo rasmi dhidi ya Rais Farmajo.

Huku wafuasi wa waziri mkuu huyo wa Somalia, akiwemo Msaidizi wa Waziri wa Habari nchini humo, Yusuf Omar Adala, aliyedai kuwa uamuzi huo wa Rais Farmajo, ni sawa na mapinduzi yasiyo ya moja kwa moja.

Inadaiwa kuwa, Rais Farmajo ametangaza kumsimamisha kazi Roble, siku moja tangu mwanasiasa huyo kumshutumu kwamba anakwamisha uchaguzi wa wabunge unaonedelea nchini humo.

Katika taarifa ya Ofisi ya Rais wa Somalia, imesema Roble ni tishio kwa mchakato wa uchaguzi huo, na kwamba anavuka mamlaka yake.

Hii ni mara ya pili kwa Rais Farmajo kutangaza kumsimamisha kazi Roble, ambapo mara ya kwanza alichukua hatua hiyo Mei 2021, kufuatia mgogoro wao kuhusu kukwama kwa uchaguzi wa wabunge.

Hata hivyo, Roble alijibu tuhuma hizo kupitia ofisi yake, akidai kwamba Rais Farmajo ndiye anayetumia nguvu kubwa na rasilimali fedha kuvuruga uchaguzi huo.

Kupitia taarifa yake, Roble alisema atafafanya mikutano kutafuta njia za kuharakisha uchaguzi huo .

Imeripotiwa kuwa, uchaguzi wa wabunge ulioanza Novemba Mosi mwaka huu, ulipaswa kufika tamati tarehe 24 Desemba 2021, lakini hadi sasa haujaisha huku wabunge 24 ndiyo waliochaguliwa kati ya wabunge 275 wanaotarajiwa kuchaguliwa.

Ukurasa wa Twitter wa Ofisi ya Waziri Mkuu wa Somalia, leo Jumatatu imeandika ukidai kuwa, uamuzi wa Rais Farmajo kumsimamisha kazi Roble unakiuka katiba ya taifa hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!