Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo yawachongea wateule wa Rais
Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yawachongea wateule wa Rais

Ado Shaibu, Katibu Mkuu ACT-Wazalendo
Spread the love

 

CHAMA cha ACT-Wazalendo, kimemuomba Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mohamed Mchengerwa, kufuatilia kwa ukaribu mienendo ya viongozi wa umma, wakiwemo wateule wa Rais, ili kuwachukulia hatua wanaokiuka misingi ya utendaji kazi wao. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Jumatatu, tarehe 27 Desemba 2021 na Naibu Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma ACT-Wazalendo, Janeth Rithe, wito huo umetolewa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Ado Shaibu, katika ziara yake kwenye Jimbo la Tunduru Kaskazini, mkoani Ruvuma.

“ Ado amemtaka Waziri Mchengerwa kufuatilia kwa karibu na kuhakikisha viongozi wanafanya kazi kwa mujibu wa sheria na misingi ya utawala bora, kwa sababu baadhi ya wakuu wa wilaya na watendaji wengine, wanatumia sana ubabe na vitisho, badala ya kuongozwa na ubunifu, maarifa na ushirikishwaji,” imesema taarifa ya Rithe.

Katika taarifa hiyo, Ado alidai, kuna baadhi ya viongozi wa umma akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Julius Mtatiro, wanakiuka maadili ya kazi kwa kutumia madaraka yao vibaya, ikiwemo kuwalazimisha wakulima wilayani humo kutoa fedha kwa ajili michango mbalimbali.

Julius Mtatiro, Mkuu wa Wilaya ya Tunduru

“Nimekwenda Tunduru Kusini na leo (jana) nipo Tunduru Kaskazini. Kote nimeelezwa kilio cha wananchi juu ya Mtatiro. Si sahihi kwa mkuu wa wilaya kuwa ubabe, kukata fedha za wakulima wa Korosho kuchangia timu ya mpira bila kushirikisha wanachama wa Vyama vya Ushirika (AMCOS),” alidai Ado na kuongeza:

“Sio sawa pia kwa mkuu wa wilaya kuingilia uendeshaji wa ushirika na kuwalazimisha wananchi kuuza mazao kwa bei ya chini. Nimeelezwa kwenye kijiji Cha Tulieni, Kata ya Nakapanya, wananchi walipigwa mabomu kwa sababu ya kutafuta bei nzuri ya mbaazi wilaya ya jirani. Masuala haya yangeweza kushughulikiwa kwa njia shirikishi, sio kwa mabomu.”

MwanaHALISI Online imemtafuta Mtatiro kwa njia ya simu, ili kupata ufafanuzi dhidi ya tuhuma hizo, ambaye amejibu kwa msisitizo kuwa hajibu propaganda.

“Sijibu propaganda mimi, sijibu propaganda,” amejibu Mtatiro.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!