Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia: Wanasiasa tusiburuze wananchi mchakato wa katiba mpya
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia: Wanasiasa tusiburuze wananchi mchakato wa katiba mpya

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan amevitaka vyama vya siasa kutohodhi mchakato wa marekebisho ya katiba, akisema suala hilo si mali yao bali ni mali ya wananchi wote. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Akifungua mkutano maalum wa Baraza la Vyama vya Siasa, leo tarehe 11 Septemba 2023, jijini Dar es Salaam, Rais Samia amewataka wanasiasa kutowaburuza wananchi kuhusu mabadiliko ya katiba.

Mkuu huyo wa nchi, amesema mchakato huo utaanza na utoaji elimu kwa wananchi ili waielewe katiba, kwa kuwa asilimia kubwa hasa walioko vijijini hawaijui vyema.

“Tunaanza na elimu ya katiba, watanzania wajue ni kitu gani, wajue kinasemaje na kina nini sababu tunakokwenda viongozi wa kisiasa tunadhani tuna haki ya kuburuza watu.

Tunachokisema sisi watu wote wafanye hivyo. Katiba si kitabu ni morality ethical standard, tutaenda kwa mwendo huu kila mtu ajue,”amesema Rais Samia.

Rais Samia amesema “tuna kazi kubwa ya kuwafanya watanzania waijue katiba ni nini na hiko kitabu kimekaaje. Wengine hawakijui ukienda huko vijijini mtu anaweza akaja na Ilani ya CCM akakwambia katiba, hajui ilani inasemaje wala katiba inasemaje hawajui.”

Katika hatua nyingine, Rais Samia amesema kamati maalumu itaanzishwa kwa ajili ya kusimamia mchakato huo, ambapo vyama vya siasa vitatoa uwakilishi wake.

“Tusiwaburuze, katiba viongozi wa siasa si yetu ni mali ya watanzania. Mwisho wa mkutano huu nimemwambia msajili nataka viongozi wa vyama walete maoni yao kwenye kamati itakayokwenda kuanzisha mchakato wa katiba na ninyi mtakuwa na wawakilishi wenu sio kila mtu ataingia kule,” amesema Rais Samia.

Msimamo wa Rais Samia kuanza kutoa elimu kwa wananchi juu ya katiba, umepinga vikali na baadhi ya makundi ikiwemo asasi za kiraia, ambayo yameshauri mchakato huo uanze moja kwa moja katika marekebisho kwa madai kuwa elimu ilishatolewa hapo awali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!