Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia kuteta na wanawake Dodoma kesho
Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuteta na wanawake Dodoma kesho

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kesho Jumanne, tarehe 8 Juni 2021, kuanzia saa 3:00 asubuhi, atazungumza na wanawake wa mkoa wa Dodoma. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Ni katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete Convertion Center, uliopo jijini Dodoma.

Akizungumzia mkutano huo, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Anthony Mtaka amesema, Rais Samia atazungumza na wanawake zaidi ya 10,000 wakiwakilisha wanawake wote nchini.

Anthony Mtaka, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma

Mtaka amesema, wanawake wa Wilaya ya Dodoma na maeneo jirani, wamekwisha kupewa mwaliko wa kuhudhuria mkutano huo pamoja na wabunge wanawake bila kujali vyama vyao wamealikwa kushiriki.

Hii itakuwa mara ya pili, Rais Samia kukutana na kuzungumza na makundi maalum, ikitanguliwa na mazungumzo aliyoyafanya na Wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam hivi karibuni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

error: Content is protected !!