Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Elimu bure yaibua tena bungeni, Serikali yatoa majibu
Habari Mchanganyiko

Elimu bure yaibua tena bungeni, Serikali yatoa majibu

David Silinde, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Spread the love

 

MBUNGE wa Nkasi Kaskazini (Chadema), Aida Khenani, ameihoji Serikali ya Tanzania, kwa nini wanafunzi wameendelea kuchangishwa michango wakati “inasema elimu ya Shule ya msingi na sekondari ni bure? Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Aida, amehoji hilo, leo Jumatatu, tarehe 7 Juni 2021, bungeni jijini Dodoma, wakati wa kipindi cha maswali na majibu.

“Je, kwa nini Wazazi wanachangishwa michango ya kuchangia elimu wakati Serikali inasema elimu ya Shule ya Msingi na Sekondari ni bure,” amehoji Aida

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Tamisemi, David Silinde amesema, Serikali kupitia Waraka wa Elimu Namba 5 wa mwaka 2015 iliamua kutoa Elimumsingi bila malipo kuanzia Elimu ya awali hadi Kidato cha Nne.

“Uamuzi huo ulijielekeza katika kutekeleza Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 ambayo ina lengo la kuhakikisha watoto wote wa Kitanzania wenye rika la Elimumsingi wanapata Elimu bila kikwazo chochote ikiwemo Ada au michango,” amesema

Silinde amesema, Serikali ilitoa Waraka wa Elimu Namba 3 wa mwaka 2016 kuhusu utekelezaji wa Elimumsingi Bila Malipo.

“Waraka huu unafafanua maana ya Elimumsingi na kuainisha majukumu ya kila kundi linalohusika katika utoaji wa Elimumsingi bila malipo na kuweka utaratibu wa utekelezaji wake,” amesema

Aida Khenan, Mbunge wa Nkasi Kaskazini (Chadema)

Silinde amesema, majukumu ya jamii na wananchi kuhusu michango yamebainishwa kwenye Waraka wa Elimu Namba 3 wa mwaka 2016.

Amesema, Waraka unaeleza kuwa Kamati za Shule au Bodi za Shule zitashirikisha jamii katika maazimio na maamuzi ya masuala mbalimbali yanayohusu maslahi na maendeleo ya shule hususan uchangiaji wa hiari na kuwasilisha maamuzi hayo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ili kupata kibali.

“Hivyo, uchangiaji katika elimu unaoruhusiwa ni wa hiari na hauhusishi wanafunzi kuzuiwa kuhudhuria masomo,” amesema

Kwa upande wake, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amesema, kuna michango ya hiari ambayo kupitia kamati za shule, wazazi wana ridhia na kuchangia.

Swali kama hilo la Aida, si la kwanza kuulizwa bungeni, limekuwa likiulizwa mara kwa mara hasa michango inayochangishwa wakati elimu ni bure.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!