WAKATI Ligi Kuu Tanzania Bara inaelekea ukingoni huku kukiwa na vita tatu tofauti katika maeneo mablimabli kwenye msimu huu wa 2020/21, huku vita inayoangaliwa kwa sasa ni vita ya upachikaji mabao kati ya John Bocco mshambuliaji wa Simba pamoja na Prince Dube kutoka Azam Fc. Anaripoti Mwandishi Wetu
Wawili hao wameingia kwenye vita ya kunyakuwa kiatu cha mfungaji bora mara baada ya kupishana kwa bao moja katika msimamo wao.
Prince Dube kutoka Azam FC yupo kileleni akiwa na jumla ya mabao 14 aliyocheza akiwa na Azam FC toka alijiunga nayo mwanzoni mwa msimu huu wa 2020/21.
Nafasi ya pili inashikiliwa na John Bocco ambaye amekuwa na moto mkali toka aliporudi kutoka kwenye majeraha nakufikisha jumla ya mabao 13.
Wawili hao walikuwa kwenye majeruhi katika kipindi tofauti lakini walirejea wakiwa na makali yao ya kufumania nyavu katika michezo ya Ligi Kuu.
Katika michezo yake mine toka aliporejea kutoka kwenye majeruhi John Bocco amepachika jumla ya mabao saba na kuwa mshambuliaji kinara wa mabao ndani ya klabu ya Simba na kupachika mabao Zaidi ya 12 katika kipindi cha misimu saba.
Ukiachia Ligi Dube mpaka sasa amepachika jumla ya mabao 17 katika michezo 27 aliyoichezea Azam Fc katika michuano tofauti kiasi cha kuwavutia matajiri wa timu hiyo kumpa mkataba mpya utakaomfanya aendelee kusalia hadi 2024.
Leave a comment