Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia awageuzia kibao watumishi wa umma
Habari za Siasa

Rais Samia awageuzia kibao watumishi wa umma

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu, amewaagiza viongozi wa mikoa, wilaya na halmashauri, kutowafumbia macho watumishi wa umma wanaojihusisha na vitendo vya wizi, uzembe na upotevu wa fedha kazini. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Rais Samia ametoa agizo hilo leo Jumatatu, tarehe 18 Oktoba 2021, katika ziara yake ya kikazi wilayani Longido, Mkoa wa Arusha.

“Kuna vitendo vya watu kutowajibika kazini, wizi, upotevu wa mapato, uzembe bado mnaoneleana… shida hamchukui hatua, niombe halmashauri simamieni, piganeni na vitendo hivi. Wakuu wa mikoa, wilaya na wakurugenzi kasimamieni hayo,” amesema Rais Samia.

Aidha, Rais Samia amewaagiza madiwani kusimamia mapato na matumizi ya fedha za halmashauri zao.

“Madiwani Serikali imebeba posho zenu, la kwenu kusimamia maendeleo, makusanyo na matumizi mazuri ya fedha nidhamu katika maeneo yenu,” amesema Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

7 wafa Ulanga, mbunge alia kutelekezwa na mawaziri, Tanroad

Spread the loveWatoto saba wamepoteza maisha na zaidi ya kaya 70 kukosa...

Habari za SiasaTangulizi

Wizara Katiba na Sheria yaliomba Bunge Sh. 441.2 bilioni

Spread the love  WIZARA ya Katiba na Sheria imeliomba Bunge liidhinishe bajeti...

error: Content is protected !!